Wednesday , 1 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Rungwe kuzindua kampeni J’mosi Dar, aahidi ubwabwa
Habari za Siasa

Rungwe kuzindua kampeni J’mosi Dar, aahidi ubwabwa

Spread the love

MGOMBEA urais wa Tanzania kupitia Chama cha Chaumma, Hashimu Rungwe, ametangaza kuzindua kampeni zake za urais wa chama hicho Jumamosi tarehe 5 Septemba 2020 Manzese jijini Dar es Salaam. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea)

Rungwe ambaye ni Mwenyekiti wa Chaumma amesema hayo leo Jumatatu tarehe 31 Agosti 2020 alipokuwa akizungumza na MwanaHALISI Online lililotaka kujua uzinduzi wa kampeni zake.

“Chaumma itaongea na wananchi 5 Septemba 2020 katika Uwanja wa Manzese Dar es Salaam kuanzia saa 8 mchana. Wananchi waje wasikilize, tunachowaambia. Wakija pale watapata kila kitu na watauliza maswali na tutawajibu,” amesema Rungwe

“Wako watu wenye hamu ya ubwabwa waje tutajua tunawapatiaje,” amesema

Rungwe ameahidi endapo akiingia madarakani baada ya uchaguzi mkuu utakaofanyika Jumatano tarehe 28 Oktoba 2020, atarejesha mfumo wa zamani wa kugawa chakula kwa wanafunzi shuleni.

Amesema, Serikali atakakayoiunda itahakikisha inagawa wali (ubwabwa) kwa wanafunzi shuleni ili kuwawezesha kusoma na kuwawezesha kufaulu vyema masomo yao.

Rungwe amesema, hakuna mtu asiyependa ubwabwa na Serikali yake itahakikisha hilo linafanyiwa kazi kwani mtu akishiba anaweza kufanya kazi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari za Siasa

Mavunde aomba bilioni 231.9 bajeti wizara ya madini

Spread the loveWAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde leo Jumanne amewasilisha hotuba ya...

Habari za SiasaTangulizi

Lissu amjibu Fatma Karume kuhusu Rais Samia

Spread the love  MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)...

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Slaa: Watanzania iungeni mkono Chadema uchaguzi 2025

Spread the loveMWANASIASA mkongwe nchini Tanzania, Dk. Wilbroad Slaa, amewataka watanzania wakiunge...

error: Content is protected !!