Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari Rais Samia: Dk. Mwigulu uwe mwepesi
Habari

Rais Samia: Dk. Mwigulu uwe mwepesi

Spread the love

 

RAIS Samia Suluhu Hassan amemuagiza Waziri wa Fedha na Mipango, Dk. Mwigulu Nchemba kuthibiti urasimu wa kupata msamaha wa kodi kwa vifaa na bidhaa zitakazoagizwa kutoka nje ya nchi katika miradi inayotekeleza chini ya mpango wa fedha zilizotolewa na Shirika la Fedha Duniani (IMF) kwa Tanzania. Anaripoti Mwandishi wetu (endelea)

Rais Samia ametoa kauli hiyo leo tarehe 10 Oktoba, 2021 jijini Dodoma wakati akizindua kampeni ya maendeleo kwa ustawi na mapambano ya UVIKO -19 ambao umetokana na mkopo nafuu wa Sh trilioni 1.3 uliotolewa na Shirika hilo la IMF.

“Nakuagiza kusimamia suala hili, kuwa mwepesi kutoa misamaha ya kodi kwa yale yatakayoagiza kuja kutumika kwenye miradi hii,” alisema.

Pia amemuagiza Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali na Mkaguzi wa ndani wa hesabu za serikali kufuatilia kwa karibu matumizi ya fedha hizo ili kuhakikisha zinatumika kwa malengo yaliyokusudiwa na thamani halisi yaani ‘value for money’

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

HabariSiasa

Dk. Rose Rwakatare atoa kadi 500 kila Wilaya Morogoro

Spread the loveMWENYEKITI wa Jumuiya ya Wazazi CCM Mkoa wa Morogoro, Dk...

ElimuHabari

CBE, WMA wasaini makubaliano wanafunzi kusoma wakifanyakazi

Spread the loveNAIBU Spika Musa Azzan Zungu amekipongeza Chuo cha Elimu ya...

HabariTangulizi

Dk. Slaa, Mwabukusi kuhojiwa na jeshi la Polisi Mbeya

Spread the loveJESHI la Polisi jijini Mbeya, linawashikilia kwa mahojiano Dk. Wilbroad...

HabariHabari Mchanganyiko

Kairuki Hospital Green IVF  yawanoa madaktari kuhusu upandikizaji mimba

Spread the love KITUO cha Upandikizaji Mimba cha Kairuki Hospital Green IVF...

error: Content is protected !!