Friday , 19 April 2024
Home Gazeti Habari ‘Mnasema Rais ni mweupe! dokoa pesa muone rangi halisi’ – Rais Samia
Habari

‘Mnasema Rais ni mweupe! dokoa pesa muone rangi halisi’ – Rais Samia

Rais Samia Suluhu Hassan
Spread the love

 

RAIS Samia amewaonya viongozi, watumishi na wazabuni watakaosimamia miradi itakayotekelezwa kwa kutumia fedha zilizotolewa na Shirika la Fedha Duniani (IMF) kwa Tanzania, basi wajaribu kudokoa fedha hizo. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea)

Rais Samia ametoa kauli hiyo leo tarehe 10 Oktoba, 2021 jijini Dodoma wakati akizindua mpango wa kampeni ya maendeleo kwa ustawi na mapambano ya UVIKO -19 ambao umetokana na mkopo nafuu wa Sh trilioni 1.3 uliotolewa na Shirika hilo la IMF.

“Hili niliseme tu kwa wale wanaotaka kuzijua rangi zangu halisi mkinitazama hivi mnasema Rais ni mweupe lakini nina rangi halisi, kwa wale wanaotaka kujua rangi zangu halisi, wajaribu kudokoa pesa hizi au wabadilishe matumizi ya pesa hizi bila maelewa,” amesema.

Aidha, amesema kutokana na mpango huo nchi inakwenda kuchemka, kila kona kutakuwa na ujenzi, miradi ya maendeleo hivyo wakurugenzi wa halmashauri na wasaidizi wao wasimamie miradi hiyo ipasavyo kuhakikisha fedha hii inatumika ipasavyo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

HabariSiasa

Dk. Rose Rwakatare atoa kadi 500 kila Wilaya Morogoro

Spread the loveMWENYEKITI wa Jumuiya ya Wazazi CCM Mkoa wa Morogoro, Dk...

ElimuHabari

CBE, WMA wasaini makubaliano wanafunzi kusoma wakifanyakazi

Spread the loveNAIBU Spika Musa Azzan Zungu amekipongeza Chuo cha Elimu ya...

HabariTangulizi

Dk. Slaa, Mwabukusi kuhojiwa na jeshi la Polisi Mbeya

Spread the loveJESHI la Polisi jijini Mbeya, linawashikilia kwa mahojiano Dk. Wilbroad...

HabariHabari Mchanganyiko

Kairuki Hospital Green IVF  yawanoa madaktari kuhusu upandikizaji mimba

Spread the love KITUO cha Upandikizaji Mimba cha Kairuki Hospital Green IVF...

error: Content is protected !!