Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Tangulizi Rais Samia ateua viongozi akiwa Malawi
Tangulizi

Rais Samia ateua viongozi akiwa Malawi

Rais Samia Suluhu Hassan
Spread the love

 

RAIS wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, amefanya uteuzi wa viongozi mbalimbali leo Jumanne, tarehe 17 Agosti 2021. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Taarifa iliyotolewa na Jaffar Haniu, Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu imewataja walioteuliwa kuwa; ni Jaji Mkuu mstaafu Mohamed Chande Othman kuwa Mkuu wa Chuo Kikuu cha Ardhi (ARU).

Rais Samia, amefanya uteuzi huo akiwa nchini Malawi anakoendelea kushiriki mkutano wa 41 wa Wakuu wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC).

Mkutano huo, umeanza leo Jumanne na utamazilika kesho Jumatano.

Pia, amemteua Prof. Elisante Ole Gabriel kuwa Mtendaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania.

Kabla ya uteuzi huo, Prof. Ole Gabriel alikuwa Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (upande wa Mifugo) ambaye anachukua nafasi ya Mathias Kabunduguru ambaye amestaafu.

Haniu amesema, Prof. Ole Gabriel ataapishwa tarehe 21 Agosti, 2021, saa 03:00 asubuhi Ikulu Jijini Dar es Salaam pamoja na Mabalozi Wateule watatu.

Mabalozi hao; ni Lt. Jen. Yakub Hassan Mohamed kuwa Balozi wa Tanzania nchini Uturuki, Balozi mteule Mahmoud Thabit Kombo kuwa Balozi wa Tanzania nchini Italia na Balozi Mteule Elsie Sia Kanza kuwa Balozi wa Tanzania nchini Marekani.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari za SiasaTangulizi

Mpwa wa Magufuli mbaroni kwa kusambaza picha za utupu

Spread the loveJESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata...

Habari za SiasaTangulizi

Shibuda amlima waraka mzito Bulembo

Spread the loveMKONGWE wa siasa nchini, John Shibuda amemshukia kada maarufu wa...

error: Content is protected !!