Wednesday , 17 April 2024
Home Kitengo Michezo Simba yatambulisha mwingine
Michezo

Simba yatambulisha mwingine

Spread the love

 

KLABU ya Simba imefanikiwa kunasa saini ya kiungo mshambuliaji wa klabu ya Kagera Sugar, Abdulsamad Kassim mwenye umri wa miaka 24. Anaripoti Mintanga Hunda TUDARCo…(endelea)

Mchezaji huyo ambaye alikuwa moja ya wachezaji nyota ndani ya kikosi cha Kagera Sugar amejiunga na Simba kwa mkataba wa miaka miwili.

Abdulsamad ametambulishwa ndani ya klabu hiyo, huku akiwa sehemu ya kikosi hiko kilichopo nchini Morocco kwenye maandalizi (Pre-Season), kuelekea msimu mpya wa mashindano 2021/22.

Simba imeongeza idadi ya kiungo mara baada ya kuondoka kwa Clatous Chama, aliyetimkia nchini Morocco kwenye klabu ya RS Berkane kwa mkataba wa miaka mitatu.

Huu utakuwa usajili wa saba kutambulishwa na klabu ya Simba toka kufunguliwa kwa dirisha kubwa la usajili ambapo litafungwa Agosti 30, mwaka huu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Leo ni leo nani kutinga nusu fainali UEFA?

Spread the love HATIMAYE Jumanne ya UEFA imefika ambapo leo hii michezo...

Michezo

Anza Jumatatu yako na Meridianbet

Spread the love  IKIWA ni siku nyingine mpya kabisa ya Jumatatu baadhi...

Habari MchanganyikoMichezo

NBC, Yanga wazindua kadi  za kimataifa za uanachama

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) kwa kushirikiana na Klabu...

Michezo

TFF, Amrouche ngoma nzito

Spread the loveVIPENGELE vya mkataba wa kazi aliotia saini Kocha Mkuu wa...

error: Content is protected !!