RAIS Samia Suluhu Hassan amemteua Balozi Khamis Sued Kagasheki kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Parole kuanzia tarehe 18 Aprili 2023.
Awali nafasi hiyo ilikuwa inashikiliwa na aliyekuwa Mwenyekiti wa Chama cha TLP, Agustine Mrema ambaye alifariki dunia tarehe 16 Agosti 2022.
Mrema alikuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Parole tangu mwaka 2016 alipoteuliwa na Rais wa awamu ya tano, Dk. John Magufuli.
Leave a comment