Sunday , 28 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Samia akutana na Papa Francis
Habari za Siasa

Rais Samia akutana na Papa Francis

Spread the love

Rais Samia Suluhu Hassan, leo Jumatatu tarehe 12 Februari 2024 amekutana na Kiongozi mkuu wa Kanisa Katoliki duniani, Papa Francis katika mji wa Vatican kuteta mambo manne muhimu. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Rais Samia pia amekutana na Katibu Mkuu wa Vatican, Kadinali Pietro Parolin na viongozi wengine akiwemo Askofu Paul Richard Gallagher anayeshughulikia uhusiano wa Vatican na mataifa mbalimbali duniani.

Papa Francis alimpokea Rais Samia mara baada ya kuhudhuria misa takatifu katika Kanisa la Mtakatifu Peter (St Peter’s Basilica.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Vatican imeeleza kuwa mazungumzo hayo yaliangazia kuendeleza mahusiano mazuri yaliyopo kati ya Tanzania na Vatican.

“Hayo yanatokana na namna Kanisa Katoliki linavyotumia muda mwingi katika kuboresha nyanja za elimu na afya pamoja na kutoa misaada nchini Tanzania.

“Majadiliano pia yalilenga kuimarisha amani kati ya nchi zote mbili,” imesema.


Rais Samia ameanza ziara yake huko Vatican kwa siku mbili kuanzia tarehe 11 na 12 Februari mwaka huu. Tarehe 13 Februari, Rais Samia atawasili Norway kwa ziara nyingine ya siku mbili.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde aibana kampuni kutimiza masharti ya mkataba

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameitaka Kampuni ya Xin Tai...

Habari za Siasa

Sauti ya Watanzania waeleza sababu za kuiunga mkono Chadema

Spread the love  KIKUNDI kinachojipambanua katika kupigania rasilimali na uhuru wa nchi,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

error: Content is protected !!