Friday , 3 May 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Rais Ruto amtolea uvivu Kenyatta, amuonya ukaribu na Odinga
KimataifaTangulizi

Rais Ruto amtolea uvivu Kenyatta, amuonya ukaribu na Odinga

Spread the love

RAIS wa Kenya William Ruto amedai kuwa aliyekuwa mtangulizi wake Uhuru Kenyatta anajaribu kubomoa serikali yake kwa kufadhili maandamano. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa…(endelea).

Akizungumza katika ziara yake kwenye Mji Mai Mahiu nchini humo, Ruto alidai kuwa Uhuru alikuwa anafadhili vijana wa Mungiki kusababisha vurugu wakati wa maandamano ya Azimio la Umoja One Kenya Coalition Party.

Ruto alionya kuwa ikiwa rais huyo wa zamani hatasitisha ufadhili wa shughuli za Azimio, atalazimika kuchukua hatua dhidi yake.

Ruto alimtaka rais wa zamani kuwa mwanamume, akidai kwamba walimuunga mkono alipokuwa kwenye uongozi wa nchi.

Kiongozi huyo wa taifa alimtaka Uhuru aache kujiunganisha na kiongozi wa ODM, Raila Odinga, ambaye aliahidi kumzuia kwenye makazi yake ya mashambani.

“Nataka pia kumwomba rafiki yangu Uhuru ajiweke mbali na yule Mzee (Raila). Acha kumpa pesa ya kuajiri Mungiki kuharibu Nairobi. Wewe ulikuwa rais, kuwa mwanamume. Tulikusaidia ulipokuwa rais. Ikiwa hautajitenga naye, tutakutuma mbali pia, kama vile huyo mtu wa mafumbo,” alisema Ruto.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Sabaya afutiwa kesi, ruksa kugombea uongozi

Spread the loveMwendesha Mashtaka Mkuu wa Serikali DPP leo Ijumaa amefuta rufaa...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kwafukuta kisa chaguzi, Lissu aibua tuhuma nzito

Spread the loveCHAGUZI za kusaka viongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo...

Habari MchanganyikoTangulizi

Kimbunga “HIDAYA” chaendelea kuimarika, wananchi wapewa tahadhari

Spread the loveMAMLAKA ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) inaendelea kutoa taarifa...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kumshtaki Rais Samia

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimetishia kumfungulia kesi ya...

error: Content is protected !!