Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Mwinyi ateua makatibu wakuu wannne
Habari za Siasa

Rais Mwinyi ateua makatibu wakuu wannne

Dk. Hussein Ali Mwinyi, Rais wa Zanzibar
Spread the love

 

RAIS wa Zanzibar, Dk. Hussein Ali Mwinyi, ameteua makatibu wakuu wanne, wa wizara na taasisi mbalimbali visiwani humo. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam…(endelea).

Taarifa ya uteuzi huo imetolewa leo Ijumaa, tarehe 30 Julai 2021 na Katibu Mkuu Kiongozi Zanzibar, Mhandisi Zena Said.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, Rais Mwinyi amemteua Dk. Fatma Mrisho, kuwa Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Ustawi wa Jamii, Wazee, Jinsia na Watoto. Huku Khadija Khamis Rajab, akiteuliwa kuwa Katibu Mkuu, anayeshughulikia masuala ya kazi na uwezeshaji, katika Ofisi ya Rais, Kazi, Uchumi na Uwezeshaji.

“Dk. Habiba Hassan Omar, ameteuliwa kuwa Katibu Mkuu anayeshughulikia masuala ya uchumi na uwekezaji, katika Ofisi ya Rais, Kazi, Uchumi na Uwekezaji,” imesema taarifa hiyo.

Dk. Omar Dadi Shajak, ameteuliwa na Rais Mwinyi kuwa, Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais, visiwani humo.

Taarifa ya Mhandisi Zena imesema kuwa, wateule hao wataapishwa Jumatatu, tarehe 2 Agosti 2021, Ikulu visiwani Zanzibar.

Pia, taarifa hiyo imesema, siku hiyo Rais Mwinyi atamuapisha Khamis Kona Khamis, aliyemteua kuwa Mkurugenzi wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC). Khamis aliteuliwa kushika wadhifa huo tarehe 16 Julai mwaka huu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!