Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Kamati Kuu CCM yaagiza watovu wa nidhamu washughulikiwe
Habari za SiasaTangulizi

Kamati Kuu CCM yaagiza watovu wa nidhamu washughulikiwe

Shaka Hamdu Shaka, Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM
Spread the love

 

KAMATI Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), imeelekeza makada wake wanaokiuka mienendo na maadili ya chama hicho, wachukuliwe hatua za kinidhamu. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Taarifa hiyo imetolewa tarehe 29 Julai 2021 na Katibu wa Itikadi na Uenezi CCM, Shaka Hamdu Shaka, akitoa maazimio ya kikao maalumu cha kamati hiyo, kilichofanyika jana jijini Dar es Salaam.

Shaka alisema, kamati hiyo imeeleza wanachama hao waanze kuchukuliwa hatua, kwa mujibu wa katiba ya CCM.

Rais Samia Suluhu Hassan, Mwenyekiti wa CCM

“Kamati Kuu imeeleza kuanza kuchukuliwa hatua kwa wale wote wanaokiuka mienendo, taratibu na kanuni za maadilina uongozi kwa mujibu wa katiba ya chama,” alisema Shaka.

Malekezo ya kamati hiyo yamekuja katika kipindi ambacho kuna mvutano kati ya Mbunge wa Kawe (CCM), Askofu Josephat Gwajima na Serikali ya Rais Samia Suluhu Hassan, kuhusu mpango wa kuwachanja wananchi chanjo ya Ugonjwa wa Korona (UVIKO-19).

Hivi karibuni, Askofu Gwajima alitangaza hadharani kupinga mpango huo, kwa madai kuwa una madhara kwa afya za Watanzania.

Hata hivyo, Serikali imekanusha madai hayo ikisema kwamba chanjo hizo ni salama.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!