Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Magufuli kukabidhi uenyekiti SADC J’tatu
Habari za Siasa

Rais Magufuli kukabidhi uenyekiti SADC J’tatu

Rais John Magufuli, Mwenyekiti wa Jumuiya ya SADC akihutubia wajumbe wa mkutano huo
Spread the love

RAIS wa Tanzania, John Pombe Magufuli anakabidhi rasmi kijiti cha Uenyekiti wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC), kwa Rais wa Msumbiji, Phillip Nyusi, Jumatatu tarehe 17 Agosti 2020. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Rais Magufuli anakabidhi uenyekiti huo wa SADC kwa Rais Nyusi, baada ya kumaliza muda wake wa mwaka mmoja wa kuongoza jumuiya hiyo, tangu alipokabidhiwa rasmi na Rais wa Namibia, Hage Geingob Agosti 2019.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Jumamosi tarehe 15 Agosti 2020 na Dk. Hassan Abbasi, Msemaji Mkuu wa Serikali ya Tanzania amesema baada ya mwaka mmoja wa mafanikio na kazi kubwa ya kuongoza jumuiya muhimu katika ukanda wa Afrika SADC, Rais Magufuli atakabidhi kijiti kwa mafanikio makubwa kwa Rais Phillip Nyusi.

Dk. Abbasi amesema, katika makabidhiano hayo, Rais Magufuli ataeleza kwa kina mafanikio ya Tanzania katika kuiongoza jumuiya hiyo.

“Rais Magufuli yeye mwenyewe ataeleza mafanikio kwa kina ya ajenda gani tuliisukuma na maamuzi gani yamefanyika kataika jumiya ya SADC na yamekuwa na manufaa gani kwa wananchi wa nchi 15 za jumuiya hiyo,” amesema Dk. Abbasi.

Makabidhiano ya Unyekiti wa SADC kwa Nchi ya Msumbiji yalianza wiki iliyopita, ambapo Alhamisi tarehe 13 Agosti 2020 , Prof. Palamagamba Kabudi, Waziri wa Mambo ya Nje wa Tanzania, alikabidhi uenyekiti wa Baraza la Mawaziri wa SADC, kwa Waziri wa Mambo ya Nje wa Msumbiji, ambaye aliwakilishwa na Balozi wa taifa hilo nchini Tanzania, Monica Clemente.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Sauti ya Watanzania waeleza sababu za kuiunga mkono Chadema

Spread the love  KIKUNDI kinachojipambanua katika kupigania rasilimali na uhuru wa nchi,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

error: Content is protected !!