Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Magufuli ahamia rasmi Dodoma
Habari za Siasa

Rais Magufuli ahamia rasmi Dodoma

Rais John Magufuli akijiandikisha kwenye daftari ya kupiga kura katika makazi yake mpya Chamwino, Jijini Dodoma
Spread the love

RAIS John Magufuli ametangaza kuhamia rasmi kwenye Ikulu ya Chamwino, jijini Dodoma. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Taarifa hiyo imetolewa na Gerson Msigwa, Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu, leo tarehe 12 Oktoba 2019.

Taarifa ya Msigwa imesema Rais Magufuli ametangaza uamuzi huo, alipokwenda kujiandikisha katika orodha ya wapiga kura ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa, kwenye Kituo cha Sokoine wilayani Chamwino, Dodoma. 

Rais Magufuli ameeleza kuwa, kuanzia sasa shughuli zake atazifanyia jijini humo.

“Mimi nilikuwa Katavi, nimeamua kuja kujiandikisha nyumbani sababu hapa ndio nyumbani kwangu, na nimeshakuja rasmi hapa. Kwa hiyo kila siku tutakuwa tunaonana hapa. Ndio maana nimeona nije nijiandikishe mimi pamoja na mke wangu,” amesema Rais Magufuli.

Rais Magufuli amehamia jijini Dodoma akitokea Ikulu ya Dar es Salaam, waliyokokaa watangulizi wake, Rais wa Awamu ya Kwanza, Mwalimu Julius Nyerere hadi Rais wa Awamu ya Nne, Dk. Jakaya Kikwete.

Ikulu hiyo ilijengwa na Wajerumani mwaka 1891 kabla ya Tanzania Bara (Tanganyika) kupata uhuru, tarehe 9 Desemba 1961, na kuungana na Zanzibar mwaka 1964 na kuwa nchi ya Tanzania.

Rais Magufuli amehamia Dodoma ili kumuenzi Mwalimu Nyerere, aliyeanzisha wazo la Makao Makuu ya Nchi kuwa jijini humo.

Kuhusu zoezi la uandikishaji orodha ya wapiga kura, Rais Magufuli amewahimiza Watanzania kujiandikisha, ili waweze kutumia haki yao ya kikatiba ya kuchagua viongozi wa Serikali za Mitaa watakao ona wanafaa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!