Sunday , 28 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Polisi wamhoji Wakili Dk. Nshala kwa kuzua taharuki
Habari MchanganyikoTangulizi

Polisi wamhoji Wakili Dk. Nshala kwa kuzua taharuki

Spread the love

ALIYEKUWA Rais wa Chama cha Wanasheria Tanganyika, Dk. Rugemeleza Nshala leo Alhamisi amehojiwa na katika Kituo cha Polisi Kanda Maalumu Dar Es Salaam kwa tuhuma za kutoa maneno yaliyosababisha taharuki kinyume na kifungu cha 63 C (i) cha kanuni ya adhabu. Anaripoti Mwandishi Wetu …(endelea).

Dk. Nshala ameitikia wito huo kwa mara nyingine baada ya juzi Jumanne kutohojiwa kutokana na askari aliyepangwa kumhoji kudaiwa kuwa amepata msiba.

Hata hivyo,  Dk Nshala ambaye pia ni Mkurugenzi wa Chama cha Wanasheria Watetezi wa Mazingira (LEAT), ameieleza MwanaHALISI Online kuwa amepata dhamana baada ya Polisi kufanya kazi yao Kwa weledi mkubwa.

“Tumechelewa kutoka polisi kwa sababu nyaraka za wadhamini zilikuwa na kasoro. Nshala katoa maelezo ya jina lake, anuani na makazi tu. Mengine yote kasema atayaeleza mahakamani,” ameeleza Wakili wa Dk. Nshala, Hekima Mwasipu.

Tarehe 21 Julai Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI), Ramadhani Kingai aliwaita baadhi ya watu kuhojiwa na polisi akidai kuwa walitoa maneno yenye viashiria vya uchochezi na matumizi ya lugha  za kifedhuli kwa viongozi.

Miongoni mwa walioitwa kuhojiwa na Jeshi la Polisi ni Dk. Nshala, Makamu Mwenyekiti wa Chadema, Tundu Lissu, Wakili Boniphace Mwabukusi na Maluka Nyagali ‘Mdude Nyagali’.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Mvungi aendesha kikao kazi cha wataalam wa Regrow

Spread the love  MKURUGENZI wa Idara Sera na Mipango Wizara ya Maliasili...

Habari MchanganyikoTangulizi

Jacob, Malisa waachiwa kwa masharti

Spread the love  JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

Habari Mchanganyiko

Polisi wakanusha kufanya uzembe ajali iliyouwa mwandishi Ayo Tv

Spread the loveJESHI la Polisi limekanusha tuhuma zilizoibuliwa dhidi yake  kwamba limekawia...

error: Content is protected !!