RAIS wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan amewaapisha Humphrey Polepole kuwa Balozi wa Tanzania nchini Malawi na Waziri Kindamba kuwa Mkuu wa Mkoa wa Njombe. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).
Wawili hao wameapishwa leo Jumanne, tarehe 15 Machi 2022, Ikulu ya jijini Dodoma.
Polepole aliyekuwa Mbunge wa Kuteuliwa na Rais na Kindamba akiwa Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL) wameteuliwa jana Jumatatu.
Kindaba anakwenda kuchukua nafasi ya Mhandisi Marwa Rubirya aliyestaafu.
Leave a comment