Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Pigo CCM, mbunge wake afariki
Habari za Siasa

Pigo CCM, mbunge wake afariki

Marehemu Martha Jachi Umbulla
Spread the love

MARTHA Jachi Umbulla, aliyekuwa Mbunge wa Viti Maalumu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), amefariki dunia usiku wa kuamkia leo tarehe 21 Januari 2020. Anaripoti Brightness Boaz, Dar es Salaam … (endelea).

Taarifa ya kifo hicho imetolewa na Job Ndugai, Spika wa Bunge la Jamhuri kwamba, mbunge huyo alikuwa akipatiwa matibabu katika Hospitali ya HCG, Mumbai nchini India.

“Nimepokea kwa mshtuko na masikitiko makubwa taarifa za kifo cha Mhe. Martha Umbulla. Natoa pole kwa familia ya marehemu, ndugu na jamaa na wananchi wa Mkoa wa Manyara.

“Mungu awape moyo wa utulivu na subra katika kipindi hiki kigumu,” amesema Spika Ndugai na kwamba, ofisi ya bunge inaratibu mipango ya mazishi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!