Thursday , 30 March 2023
Habari Mchanganyiko

JPM amlilia mbunge wake

Rais John Magufuli
Spread the love
RAIS John Magufuli ameeleza kusikitishwa na kifo cha Martha Umbulla, mbunge wa viti maalumu kupitia ChamaCha Mapinduzi (CCM). Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Katika salamu zake za rambirambi alizozituma kwa Job Ndugai, Spika wa Bunge, Rais Magufuli ambaye ni Mwenyekiti wa CCM amesema, Umbulla alikuwa mpole, mchapakazi na mpenda maendeleo.

“Nazikumbuka jitihada zake wakati akiwa Mkuu wa Wilaya na akiwa mbunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano,” imeeleza taarifa ya Rais Magufuli iliyotolewa na Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu, Gerson Msigwa.

Martha Jachi Umbulla

Umbulla amefariki dunia usiku wa kuamkia leo tarehe 21 Januari 2020, wakati akipatiwa matibabu katika Hospitali ya HCG, Mumbai nchini India.

Taarifa ya kifo chake imetolewa na Spika Ndugai akieleza “nimepokea kwa mshtuko na masikitiko makubwa taarifa za kifo cha Mhe. Martha Umbulla. Natoa pole kwa familia ya marehemu, ndugu na jamaa na wananchi wa Mkoa wa Manyara.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

NMB Bonge la Mpango – ‘Moto Uleule’ yazinduliwa, Milioni 180…

Spread the loveMSIMU wa tatu wa Kampeni ya kuhamasisha utamaduni wa Kuweka...

Habari Mchanganyiko

Rais Samia awataka wahariri kufanya kazi bila uoga, upendeleo

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan amewataka wahariri wa vyombo...

Habari Mchanganyiko

STAMICO yasaini mkataba wa bilioni 55.2 kuchoronga miamba GGML

Spread the loveSHIRIKA la Madini la Taifa (STAMICO) limezidi kufanya vizuri katika...

Habari Mchanganyiko

NMB yatoa traksuti za Mwenge wa Uhuru Mtwara

Spread the loveBENKI ya NMB imetoa traksuti kwa mkoa wa Mtwara ambako...

error: Content is protected !!