Friday , 19 April 2024
Home Habari Mchanganyiko JPM amlilia mbunge wake
Habari Mchanganyiko

JPM amlilia mbunge wake

Rais John Magufuli
Spread the love
RAIS John Magufuli ameeleza kusikitishwa na kifo cha Martha Umbulla, mbunge wa viti maalumu kupitia ChamaCha Mapinduzi (CCM). Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Katika salamu zake za rambirambi alizozituma kwa Job Ndugai, Spika wa Bunge, Rais Magufuli ambaye ni Mwenyekiti wa CCM amesema, Umbulla alikuwa mpole, mchapakazi na mpenda maendeleo.

“Nazikumbuka jitihada zake wakati akiwa Mkuu wa Wilaya na akiwa mbunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano,” imeeleza taarifa ya Rais Magufuli iliyotolewa na Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu, Gerson Msigwa.

Martha Jachi Umbulla

Umbulla amefariki dunia usiku wa kuamkia leo tarehe 21 Januari 2020, wakati akipatiwa matibabu katika Hospitali ya HCG, Mumbai nchini India.

Taarifa ya kifo chake imetolewa na Spika Ndugai akieleza “nimepokea kwa mshtuko na masikitiko makubwa taarifa za kifo cha Mhe. Martha Umbulla. Natoa pole kwa familia ya marehemu, ndugu na jamaa na wananchi wa Mkoa wa Manyara.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

NEMC yaonya wanaojenga bila tathmini ya mazingira

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC),...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB Pesa Akaunti yawavutia wakaguzi wa ndani Afrika

Spread the loveUbunifu wa bidhaa bora wa Benki ya NMB pamoja na...

Habari Mchanganyiko

Carbon First, Ruangwa wasaini makubaliano ya biashara ya hewa ukaa

Spread the love  KAMPUNI ya Carbon First Tanzania Limited na Halmashauri ya...

Habari Mchanganyiko

CBE yawakumbuka wenye mahitaji maalum Jangwani

Spread the loveCHUO cha Elimu ya Biashara (CBE), kimetoa msaada mbalimbali na...

error: Content is protected !!