Friday , 19 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa NEC yaivimbia Marekani 
Habari za SiasaTangulizi

NEC yaivimbia Marekani 

Mwenyekiti wa NEC, Semistocles Kaijage
Spread the love

TUME ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), imeitaka Marekani kueleza namna Uchaguzi Mkuu wa Tanzania ulivyoingiliwa. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Akizungumza na gazeti moja la kila siku kuhusu kauli ya Wazir wa Mambo ya Nje ya Marekani, Michael Pompeo kuwawekea vikwazo waliohusika na kuvuruga uchaguzi huo, Jaji Semistocles Kaijage, Mwenyekiti wa NEC amesema ‘hayo ni maoni yao.’

Amesema, si vema kueleza mambo kiujumla jumla na kwamba, wanapaswa kueleza ni kwa namna gani uchaguzi mkuu wa Tanzania ulivurugwa ama kuingiliwa.

Jaji Kaijage amesisitiza, uchaguzi mkuu ulihudhuriwa na waangalizi wa nje na kuwa, kama kungekuwa na tatizo lingejionesha kwenye ripoti zao.

Taarifa ya Marekani kuweka vikwanzo kwa baadhi ya maofisa wa Tanzania bila kutaja majina, iliwekwa hadharani tarehe 19 Januari 2021.

Tamko la Pempoe limelalamikia kuwepo kwa uvunjifu wa haki za binadamu, wapinzani kuenguliwa kwenye kinyang’anyiro, kukamatwa, kunyanyaswa na hata ufungaji wa intaneti.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari za Siasa

Mavunde aagiza Perseus kuharakisha fidia Sengerema

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameipongeza Kampuni ya Perseus kwa...

Habari za Siasa

Kigogo Chadema awanyooshea vidole vigogo serikalini kuhusu ripoti ya CAG

Spread the love  MWANACHAMA wa Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Boniface Jacob, amedai...

Habari za Siasa

Wabunge waikalia kooni TAKUKURU Bungeni

Spread the love  BAADHI ya wabunge wamelia na changamoto za utendaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Mpina ataka Waziri Majaliwa ajiuzulu, akosoa teuzi za mawaziri

Spread the love  MBUNGE wa Kisesa, Luhaga Mpina, amemtaka Waziri Mkuu, Kassim...

error: Content is protected !!