Thursday , 2 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Nishati Jadidifu yapawa ajira vijana Afrika
Habari Mchanganyiko

Nishati Jadidifu yapawa ajira vijana Afrika

Spread the love

 

MATUMIZI ya Nishati jadidifu yatajwa kuwa chanzo kipya cha ajira kwa vijana nchini. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Licha ya kuongeza ajira nchini nishati hiyo itachangia kupunguza athari za mabadiliko ya tabianchi.

Hayo yameelezwa na Mkurugenzi Mtendaji mpya wa Kampuni ya CSI Energy Group, Natacha Emilien akishukuru baada ya uteuzi huo na akitaja dira ya kampuni hiyo inayojihusisha na nishati.

“Nishati mbadala hunufaisha matabaka yote ya jamii kwa usawa zaidi, hasa wajasiriamali wadogo kutokana na upatikanaji wa nishati kwa bei nafuu, kutoa mafunzo.

“Pia inasaidia katika kushirikiana na wajasiriamali wanawake kama wakandarasi wadogo katika mnyororo wa thamani,”amesema Natacha.

Akizungumza katika kongamano la mjadala wa kitaifa wa nishati safi ya kupikia uliofanyika jijini hapa Novemba 2022, Mkurugenzi wa Taasisi ya Climate Action Network Tanzania, Dk. Sixbert Mwanga alisema tafiti nyingi zinaonyesha Afrika ina kiwango kikubwa cha nishati safi inayotosheleza mahitaji ya wananchi wake.

Alisema nishati jadidifu ni chanzo kingine muhimu kitakachowezesha uzalishaji umeme bora kwa bei rahisi na kutosheleza mahitaji ya bara la Afrika.

“Nishati mbadala zilizopo ukifuatilia zinatosha na uzuri wa hizi hazihitaji kufuatwa na gridi ya Taifa, badala yake zenyewe ndiyo zinaifuata gridi ili ziende kufidia wengine wenye upungufu.”

Jitihada za Afrika katika nishati jadidifu
Wakati bosi wa CSI akitaja faida za matumizi ya nishati jadidifu kwa wananchi, Afrika miezi michache iliyopita imetoka kusaini mkataba wa Wakala wa Kimataifa wa Nishati Jadidifu (Irena) ambao utasaidia kupunguza uharibifu wa mazingira unaotokana na uzalishaji wa nishati isiyo rafiki.

Oktoba 31, 2023 Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko alitaja faida za mkataba wa Irene alipokuwa akiwasilisha azimio la mkataba huo bungeni jijini Dodoma.

Dk. Biteko alisema mkataba huo utasaidia kuimarika kwa mchango wa nishati jadidifu katika uzalishaji wa nishati ya umeme na kuliwezesha Taifa kuwa na vyanzo mchanganyiko vya umeme unaoendana na mahitaji ya ukuaji wa kiuchumi na kijamii, pia kutatua changamoto ya vyanzo vya umeme visivyo endelevu na uhakika.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB yang’ara maonesho OSHA

Spread the loveBenki ya NMB imebeba tuzo ya kampuni bora kwenye sekta...

Habari MchanganyikoKimataifa

Ruto amteua Kahariri kuwa mkuu wa majeshi

Spread the loveRAIS wa Kenya, William Ruto, amemteua Jenerali Charles Muriu Kahariri,...

Habari Mchanganyiko

Chongolo aonya viongozi vijiji kutouza NIDA kwa wageni

Spread the loveMKUU wa Mkoa wa Songwe, Daniel Chongolo amewaonya viongozi wa...

Habari Mchanganyiko

TUCTA, OSHA wataka kampuni za madini kuiga ubunifu wa GGML

Spread the loveSHIRIKISHO la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA) pamoja na Wakala...

error: Content is protected !!