Sunday , 28 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa NEC yateua 58 kugombea udiwani, ubunge Mbarali
Habari za Siasa

NEC yateua 58 kugombea udiwani, ubunge Mbarali

Sanduku la kura
Spread the love

TUME ya Taifa ya Uchaguzi, imeteua wagombea 58 kugombea ubunge wa Mbarali mkoani Mbeya pamoja na udiwani katika kata mbalimbali nchini kwenye uchaguzi mdogo unaotarajiwa kufanyika tarehe 19 Septemba 2023. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam…(endelea).

Taarifa iliyotolewa leo tarehe 22 Agosti 2023 na Kaimu Mkurugenzi wa Uchaguzi NEC, Emmanuel Kawishe wagombea hao wametoka katika vyama vya siasa 17 vilivyopata usajili kamili, ikiwemo Chama Cha Mapinduzi (CCM), ACT-Wazalendo, ADA-TADEA, ADC, Chama cha Kijamii (CCK), Demokrasia Makini, TLP na NCCR Mageuzi.

NEC imeitisha uchaguzi mdogo baada ya Mbunge wa Mbarali, Francis Mtega, kufariki dunia tarehe 1 Julai 2023, kwa ajali ya kugongwa na treka.

Katika hatua nyingine, taarifa ya Kawishe imesema kata sitazitafanya uchaguzi mdogo, ikiwemo Kata ya Nala iliyopo mkoani Dodoma. Mfaranyaki (Ruvuma), Mtyangimbole (Ruvuma), Mwaniko (Mwanza), Old Moshi Magharibi (Kilimanjaro) na Marangu Kitowo (Kilimanjaro).

“Tarehe 5 Agosti 2023, tume ilitangaza uchaguzi mdogo wa Jimbo la Mbarali na kata sita za Tanzania bara na uteuzi wa wagombea umefanyika tarehe 19 Agosti 2023, kampeni za uchaguzi zimeanza tarehe 2Agosti 2023 na zinatarajiwa kuhitimishwa tarehe 18 Septemba 2023,” imesema taarifa ya Kawishe.

1 Comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde aibana kampuni kutimiza masharti ya mkataba

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameitaka Kampuni ya Xin Tai...

Habari za Siasa

Sauti ya Watanzania waeleza sababu za kuiunga mkono Chadema

Spread the love  KIKUNDI kinachojipambanua katika kupigania rasilimali na uhuru wa nchi,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

error: Content is protected !!