Tuesday , 26 September 2023
Home Kitengo Habari Kimataifa Mwanaye rais aliyepinduliwa Gabon, afumwa na mabegi ya pesa
KimataifaTangulizi

Mwanaye rais aliyepinduliwa Gabon, afumwa na mabegi ya pesa

Spread the love

Mabegi, mifuko pamoja na masanduku yaliyojazwa fedha za nchi mbalimbali yamekutwa ndani ya nyumba ya Yann Ngulu mtoto mkubwa wa Rais Ali Bongo aliyeondolewa madarakani na Jeshi mapema wiki hii. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa …(endelea).

Hayo yamejiri siku chache baada ya Rais Ali Bongo, kuondolewa madarakani kisha Jeshi la nchi hiyo kuanza kufanya msako na upekuzi katika mali zake.

Imedaiwa kuwa mapema usiku wa kuamkia leo tarehe 31 Agosti 2023, katika nyumba ya mtoto mkubwa Yann Ngulu walikuta Mabegi, mifuko na masanduku yakiwa yamejazwa fedha.

Hata hivyo, kiasi cha pesa taslim hakijulikani kwani mifuko hiyo ilijazwa pesa za nchi tofauti tofauti za sarafu ya Dola za Marekani, Euro, na Franc.

Vyombo vya habari vya nchi hiyo vimeripoti kuwa, hatua hiyo imeibua hasira kwa raia wa nchi hiyo hasa ikizingatiwa kiongozi huyo anatuhumiwa kwa rushwa, ukosefu wa usawa wa kiuchumi na matumizi mabaya ya madaraka.

Mapema leo, Jeshi la Gabon lililompindua Rais Bongo limemteua Jenerali Brice Oligui Nguema kuwa kiongozi mpya wa nchi hiyo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Chande aliyeng’olewa TANESCO kwenda TTCL apelekwa Posta

Spread the loveRAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amemteua aliyekuwa, Mkurugenzi Mkuu wa...

Habari za SiasaTangulizi

Mgawo wa umeme wang’oa vigogo TANESCO

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amewahamisha waliokuwa vigogo wa...

Habari MchanganyikoTangulizi

Mgogoro wa ardhi Kiteto: Wakulima wadaiwa kutwanga risasi ng’ombe wa wafugaji Kiteto

Spread the loveMGOGORO kati ya wafugaji na wakulima katika Kijiji cha Lembapuli,...

Kimataifa

Uvamizi wa kijeshi Milango ya bahari ya Taiwan G7 yapinga China

Spread the loveMKUTANO wa Mawaziri wa Mambo ya nje wa nchi za...

error: Content is protected !!