ALIYEKUWA mtia nia katika kinyang’anyiro cha kuwania nafasi ya urais mwaka 2020 kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk. Mayrose Majinge ameanzisha mtandao wa kukutanisha vijana wa kiume na kike ili kuwa wachumba.
Dk. Majinge amefunguka hayo mapema wiki hii katika mahojiano Maalum na MwanaHALISI Online na TV jijini Dar es Salaam.
Dk. Majinge amesema ameanzisha program hiyo baada ya kuona jamii inapata changamoto nyingi kutokana na mapenzi.
Amesema yeye na timu yake wameanzisha ili Programu hiyo ili kupunguza migogoro inayotokana na mapenzi.
“Watu wamekuwa wakijinyonga, wakiuana kwa sababu ya mapenzi sisi tunaponya majeraha yatokanayo na mapenzi lakini pia tunakutanisha watu na kuanzisha mahusiano kwa uwiano wa sifa,” amesema.
Kwa taarifa zaidi fuatilia mahojiano hayo kwenye Mwanahalisi TV.
Leave a comment