Thursday , 2 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Msikimbilie kufanya kazi mijini – Ridhiwani Kikwete
Habari za Siasa

Msikimbilie kufanya kazi mijini – Ridhiwani Kikwete

Naibu waziri, Ofisi ya Rais, Utumishi na Utawala Bora, Ridhiwani Kikwete,
Spread the love

 

NAIBU waziri, Ofisi ya Rais, Utumishi na Utawala Bora, Ridhiwani Kikwete, amewataka watumishi wa umma, kutokimbia kufanya kazi pembezoni mwa nchi. Anaripoti Mwandishi Wetu, Pwani … (endelea).

Akizungumza na watumishi wa Halmashauri ya Chalinze, leo Jumapili, Ridhiwani alisema, “hakuna sababu ya watumishi kuchagua mahali pakufanyia kazi.”

Aliwataka watumishi wa umma, kuendelea kuwahudumia wananchi wote sawa na hakuna sababu ya kuchagua na kuweka madaraja katika utoaji wa huduma.

Alisema, “…kutochagua vituo vya kazi, kunalenga sio tu kuwasaidia baadhi, lakini kunatengeneza madaraja katika utumishi wa umma.”

Akatumia mkutano huo kuwakumbusha watumishi umuhimu wa kufanya kazi kuzingatia misingi ya kazi ikiwemo kujitambua na kutambua tunaowahudumia.

Akaongeza: “Popote utakapopelekwa kuna hadhi ya mtumishi kuweza kufanya kazi. Nawaomba wazazi kuacha kupiga simu kuwaombea watoto wenu vibali vya kuhamishwa vituo ili wapelekwe mijini.”

Katika kikao hicho, Ridhiwani aliwapongeza watumishi wa halmashauri hiyo kwa kazi nzuri wanayoifanya.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Spika Tulia aibana Serikali mafao ya wastaafu Jumuiya ya Afrika Mashariki

Spread the loveSPIKA wa Bunge, Dk. Tulia Ackson ameitaka Serikali kufanya tathimini...

Habari za Siasa

Serikali yawapa maagizo Ma-RC udhibiti magonjwa yasiyoambukiza

Spread the loveWAKUU wa mikoa nchini wametakiwa kuandaa utaratibu wa kuwawezesha wananchi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari za Siasa

Mavunde aomba bilioni 231.9 bajeti wizara ya madini

Spread the loveWAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde leo Jumanne amewasilisha hotuba ya...

error: Content is protected !!