Msajili wa Vyama vya Siasa, Jaji Francis Mutungi leo Alhamisi amekutana kwa mazungumzo na Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Freeman Mbowe na kujadili namna ya kuimarisha demokrasia nchini. Anaripoti Mwandishi Wetu …(endelea).
Mbowe ambaye pia alikuwa ameambatana na Katibu Mkuu wa chama hicho, John Mnyika pamoja na Katibu wa Baraza la Wazee (BAZECHA), Rodrick Rutembeka amekutana na Msajili baada ya kumaliza kikao chenye lengo la kuimarisha demokrasia ya vyama vingi vya siasa nchini.
Kikao hicho kilifanyika kwenye ofisi ndogo za Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa mtaa wa Shaaban Robert jijini Dar es Salaam.
Leave a comment