Saturday , 27 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Askofu Dk. Alex Malasusa mkuu wa KKKT mpya mteule
Habari MchanganyikoTangulizi

Askofu Dk. Alex Malasusa mkuu wa KKKT mpya mteule

Spread the love

Wajumbe wa Mkutano Mkuu 21 wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) wamemchagua Askofu wa Dayosisi ya Mashariki na Pwani Dk. Alex Malasusa kuwa Mkuu wa Kanisa kuchukua nafasi ya Askofu Dk. Fredrick Shoo ambaye amemaliza muda wake kikatiba. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Akitangaza matokeo ya uchaguzi huo Mwenyekiti wa uchaguzi huo, Askofu Amon Mwenda amesema Askofu Malasusa amechaguliwa jana Alhamisi baada ya kupata kura 142 akifuatiwa na Askofu wa Dayosisi ya Kaskazini Magharibi Dk. Abednego Keshomshahara aliyepata kura 96 za Wajumbe wa Mkutano.

Askofu Malasusa amechaguliwa kwa mara ya nyingine ambapo alitumikia nafasi hiyo kuanzia mwaka 2007 kabla ya kuikabidhi kwa Askofu Dk. Fredrick Shoo mwaka 2015. Kwa mujibu wa Katiba ya Kanisa haizuii Askofu aliyewahi kuwa Mkuu wa Kanisa kuchaguliwa tena.

Askofu Malasusa alizaliwa tarehe 18 April, 1961 katika kijiji cha Kiwira Wilaya ya Rungwe, Mkoa wa Mbeya. Ni mtoto wa pili katika familia ya watoto nane ya Marehemu Mchungaji Gehaz Japhet Malasusa na Subilaga Timoth Malasusa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Rais Samia kuzindua gazeti litakalotoa habari za wafanyakazi Tanzania

Spread the loveSHIRIKISHO la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), liko mbioni kufufua...

Habari Mchanganyiko

GGML yaja na teknolojia za kisasa maonesho ya OSHA Arusha

Spread the loveKATIKA kuelimisha wananchi na washiriki wa maonesho ya usalama na...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za SiasaTangulizi

Samia awataka watanzania kudumisha muungano

Spread the loveRais wa Tanzania,Samia Suluhu Hassan amewataka Watanzania kuendeleza Muungano kwa...

error: Content is protected !!