Wajumbe wa Mkutano Mkuu 21 wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) wamemchagua Askofu wa Dayosisi ya Mashariki na Pwani Dk. Alex Malasusa kuwa Mkuu wa Kanisa kuchukua nafasi ya Askofu Dk. Fredrick Shoo ambaye amemaliza muda wake kikatiba. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).
Akitangaza matokeo ya uchaguzi huo Mwenyekiti wa uchaguzi huo, Askofu Amon Mwenda amesema Askofu Malasusa amechaguliwa jana Alhamisi baada ya kupata kura 142 akifuatiwa na Askofu wa Dayosisi ya Kaskazini Magharibi Dk. Abednego Keshomshahara aliyepata kura 96 za Wajumbe wa Mkutano.
Askofu Malasusa amechaguliwa kwa mara ya nyingine ambapo alitumikia nafasi hiyo kuanzia mwaka 2007 kabla ya kuikabidhi kwa Askofu Dk. Fredrick Shoo mwaka 2015. Kwa mujibu wa Katiba ya Kanisa haizuii Askofu aliyewahi kuwa Mkuu wa Kanisa kuchaguliwa tena.
Askofu Malasusa alizaliwa tarehe 18 April, 1961 katika kijiji cha Kiwira Wilaya ya Rungwe, Mkoa wa Mbeya. Ni mtoto wa pili katika familia ya watoto nane ya Marehemu Mchungaji Gehaz Japhet Malasusa na Subilaga Timoth Malasusa.
Leave a comment