Sunday , 12 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mmoja mbaroni tuhuma za kuchoma moto gari la Lissu, uchunguzi waendelea
Habari za Siasa

Mmoja mbaroni tuhuma za kuchoma moto gari la Lissu, uchunguzi waendelea

Spread the love

 

MLINZI wa Hoteli ya Twiga, aliyefahamika kwa jina la Cyprian, anashikiliwa na Jeshi la Polisi mkoani Geita, kwa tuhuma za kuchoma gari lililokuwa linatangaza mkutano wa hadhara wa Makamu Mwenyekiti wa Chadema Bara, Tundu Lissu. Anaripoti Mwandishi Wetu, Geita … (endelea).

Taariifa hiyo imetolew leo tarehe 2 Agosti 2023 na Kaimu Kamanda wa Polisi Geita, ACP Adam Maro, baada ya gari hilo lenye usajili T.658 DQL, kuchomwa moto usiku wa kuamkia leo.

Kamanda Maro amesema uchunguzi zaidi wa tukio hilo unaendelea kufanywa na Polisi, huku akidai hadi sasa chanzo chake hakijajulikana.

Gari hilo lilikuwa linatangaza mkutano wa hadhara wa Lissu, unaotarajiwa kufanyika wilayani Chato, mkoani Geita, ambako ni nyumbani kwa aliyekuwa Rais wa Awamu ya Tano, Hayati John Magufuli.

Lissu yuko katika ziara ya kikazi Chato, ambapo hivi karibuni alitangaza nia ya kwenda kuzuru kaburi la Hayati Magufuli, ambaye alikuwa anakosoa utawala wake alipokuwa madarakani kabla hajafariki dunia Machi 2021.

1 Comment

  • Jengeni hoja mumjibu baada ya hotuba yake. Wivu na chuki za kijinga na kitoto haziinuafaishi Afrika!

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Dk. Biteko: Serikali itaendelea kushirikiana na Red Cross

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Dk.Mpango aagiza trafki kuvaa makoti ya kamera kudhibiti rushwa

Spread the loveMakamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk....

Habari za SiasaKimataifa

Palestina mwanachama wa 194 wa UN

Spread the loveBaraza Kuu la Umoja wa Mataifa jana Ijumaa limepitisha kwa...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Vijana UVCCM Kagera wataka mwenyekiti wao ajiuzulu

Spread the loveVIJANA wa Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Kagera wamemtaka Mwenyekiti...

error: Content is protected !!