MKAZI wa Kizota jijini Dodoma, Salum Jumanne Rajabu jana Alhamisi Desemba 15, 2022 alikabidhiwa pikipiki yake baada ya kushinda katika shindano la MastaBata Kote kote linaloendeshwa na Benki ya NMB. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma…(endelea).
Rajab alikabidhiwa pikipiki hiyo na Meneja wa NMB Tawi la Kambarage Jijini Dodoma Emiliana Wilson ambaye alisema mshindi huyo alipatikana katika shindano la Mastabata Kote Kote lililoendeshwa wiki iliyopita.
Akikabidhi pikipiki hiyo, Emiliana alisema ushindi katika shindano hilo siyo tatizo gumu bali siri yake ni kutumia MasterCard ya Benki ya NMB katika kufanya miamala.
Meneja alisema hadi jana shindano hilo ambalo linakwenda awamu ya tano, walishatoa zaidi ya Sh100 milioni kwa washindi 300 lakini hivi karibu wametoa pikipiki 2 na fedha kwa washindi.
“Shindano letu halibagui, tunashindanisha Wateja wetu wote wanaotumia MasterCard, wapo wanaoshinda Sh 100,000, wanaoshinda pikipiki na Wengine mwanzoni mwa Mwaka watashinda safari ya Dubai ambayo kila mshindi atakwenda na mwenza wake na kukaa huko kwa siku nne,” alisema Emiliana.
Jana, Meneja huyo alichezesha shindano hilo kutokea Dodoma ambapo mshindi wa pikipiki alipatikana Shamsanga Samu kutoka Kimara huku Sia Rajabu kutoka Msasani akiwa miongoni mwa washindi 75 waliojishindia Sh 100,000.
Meneja Mwandamizi Idara ya Fedha na uwezeshaji katika biashara za kadi kwa Benki ya NMB Erick Emmanuel alisema wataendelea kumwaga noti kwa washindi hivyo wajitokeze kushiriki.
Emanuel alisema awamu zilizotangulia zimekuwa na mafanikio makubwa ambapo washindi wametoka kila kona ya nchi hivyo mafanikio hayo yamepelekea kuanza kwa msimu wa tano ambao utaratibu wake ni kuchezesha shindano hilo kupitia matawi yake yote kwa zamu.
Akizungumza mara baada ya kukabidhi wa pikipiki yake, Salum Rajabu alisema hakutegemea kama angeshinda kwani hakuamini kama anafanya mashindano.
Rajabu alisema ni utaratibu wake kutumia Master Card kwa ajili ya kufanya miamala na kulipia huduma mbalimbali kupitia kadi yake.
“Kwamba ningeibuka mshindi hiyo sikujua, lakini pia sikujua kama nilikuwa nashindana ila napenda kutumia mfumo huu kwa sababu ni rahisi na salama zaidi, hivyo itakuwa jambo jema niseme kuwa tuendelee kutumia mafumo huu,” alisema Rajabu.
Kuhusu ushindi alisema haubagui kwani ingekuwa hivyo huenda hata yeye asingekuwa miongoni mwa washindi kwa kuwa hana uhusiano na mahusiano na wahusika zaidi ya akaunti yake ya benki anayoitegemea.
Leave a comment