Friday , 19 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Rais Marekani kufanya ziara barani Afrika
Kimataifa

Rais Marekani kufanya ziara barani Afrika

Spread the love

Rais wa Marekani, Joe Biden ameahidi kufanya ziara barani Afrika, kusini mwa jangwa la Sahara ambayo itakuwa ya kwanza tangu aliposhika wadhifa wake wa urais. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa…(endelea).

Rais Biden atafanya ziara hiyo wakati ambapo China na Urusi zinaimarisha uhusiano wa kiuchumi na kijeshi na nchi za Afrika.

Kwenye mkutano na viongozi wa nchi kadhaa za Afrika mjini Washington mapema wiki hii Biden aliahidi vitega uchumi vyenye thamani ya dola bilioni 55 kwa nchi za Afrika katika sekta za biashara na kwa ajili ya misaada ya maendeleo.

Kiongozi huyo wa Marekani pia amependekeza ushiriki wa kudumu wa Umoja wa Afrika kwenye vikao vya kundi la nchi 20 zinazoongoza kiuchumi duniani. Amesema Afrika inastahili kuwa na kiti kwenye kila sehemu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

error: Content is protected !!