Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Membe arudisha kadi ya CCM, mamia wamsindikiza
Habari za SiasaTangulizi

Membe arudisha kadi ya CCM, mamia wamsindikiza

Spread the love

BERNARD Kamillius Membe, aliyekuwa waziri wa mambo ya nje wa Tanzania, ametangaza kurejesha kadi yake ya uanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM). Anaripoti Mwandishi Wetu, Lindi … (endelea).

Membe amerejesha kadi hiyo leo Jumatatu tarehe 6 Julai 2020 nyumbani kwake Rondo mkoani Lindi.

“Leo saa 6 na nusu mchana mimi na mke wangu nikisindikizwa na mamia ya wananchi wa Rondo, tumerejesha kadi zetu za CCM kwa wenyewe.”

“Nimemwandikia KM (katibu mkuu) wa CCM kuhusu tukio hilo na kukishukuru chama kwa mema yote kilichonitendea. Nawatakia kila la heri viongozi na wanachama wote,” ameandika Membe.

Tarehe 28 Februari 2020, Kamati Kuu ya CCM ilitangaza kumfukuzwa uanachama Membe kwa madai amekuwa akikiuka taratibu na miongozo ya chama hicho tangu mwaka 2014.

Tarehe 13 Desemba 2019, Halmashauri Kuu ya CCM iliyokutana jijini Mwanza chini ya Mwenyekiti wake, Rais John Pombe Magufuli ilitoa maagizo kamati ya maadili kuwahoji Membe na makatibu wakuu wastaafu wa CCM,  Abdulrahman Kinana na Yusuf Makamba.

          Soma zaidi:-

Wakati halmashauri kuu ilitoa maagizo hayo, ililidhia msamaha uliokuwa umekwisha kutolewa na Rais Magufuli dhidi ya wabunge wake watatu, William Ngeleja (Sengerema), Nape Nnauye (Mtama) na January Makamba (Bumbuli).

Msingi wa mahojiano hayo ya sauti zao, yalitanguliwa na waraka wa Kinana na Makamba kuandika tarehe 14 Julai 2019 kwenda kwa Katibu wa Baraza la Wazee la CCM, Pius Msekwa wakidai uongozi hauwalindi dhidi ya mtu ambaye alikuwa akiwadhalilisha na walimwelezea analindwa na mtu mwenye mamlaka.

Waraka huo, ulifuatiwa na sauti za wanachama hao wasambaa mitandaoni wakizungumzia kuporomoka kwa uongozi wa CCM akiwemo Rais Magufuli.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

error: Content is protected !!