Wednesday , 29 March 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Mbunge wa CCM aikaba serikali
Habari za Siasa

Mbunge wa CCM aikaba serikali

Juma Nkamia, Mbunge wa Chemba
Spread the love

MBUNGE wa Chemba, Juma Nkamia (CCM) ameihoji serikali na kutaka ieleze ni lini itaana ujenzi wa kituo cha polisi na nyumba za askari. Anaripoti Dany Tibason … (endelea).

Nkamia aliihoji serikali leo bungeni wakati wa kipindi cha maswali na majibu kwa kutaka kujua serikali ina mpango gani wa kujenga kituo cha polisi wilayani chemba pamoja na nyumba za askari.

“Wilaya ya Chemba haina Kituo cha Polisi, Je ni lini serikali itaanza ujenzi wa kituo cha polisi na nyumba za askari,” amehoji.

Akijibu swali hilo, Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Hamad Masaun, amesema kuwa ni kweli jeshi la polisi lina uhaba wa vituo vya polisi pamoja na nyumba za kuishi askari kote nchini ikiwemo wilaya ya Chemba.

“Ili kutatua changamoto hiyo jeshi la polisi linashirikisha wananchi wa eneo husika pamoja na wadau wengine wa maendeleo ili kufanikisha azma ya serikali ya kujenga vituo vya serikali vya kisasa vya polisi pamoja na nyumba za kuishi za askari hao,” amesema Masaun.

Naibu Waziri huyo amesema Wilaya ya Chemba jeshi la polisi ka kushirikiana na kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya, wananchi na wadau wengine wapo kwenye hatua za awali za kuanza ujenzi wa kituo cha polisi.

“Kwa sasa mchoro wa ramani ya kituo na gharama za ujenzi (BOQ) vimeisha kamilika na ukusanyaji wa mahitaji ya ujenzi unaendelea,” ameeleza Masaun.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

TEMESA iliyokarabati Kivuko kwa Bil 7.5 yapata hati chafu

Spread the love  MDHIBITI na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG),...

Habari za Siasa

ACT-Wazalendo yakusanya Mil 8.5/- kodi ya zuio na kutokomea nazo

Spread the love  MDHIBITI na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG),...

Habari za Siasa

DC Kasilda Mgeni ahamasisha chakula shuleni

Spread the love  MKUU wa Wilaya ya Same, mkoani Kilimanjaro, Kasilda Mgeni...

Habari za Siasa

Bilioni 223.9 zapelekwa Tunduru ndani ya miaka 2 ya SSH

Spread the love  ZAIDI ya Sh. bilioni 223.9 zimepelekwa Wilaya ya Tunduru...

error: Content is protected !!