Thursday , 25 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mch. Msigwa aweka rehani ubunge wake kisa Makonda
Habari za SiasaTangulizi

Mch. Msigwa aweka rehani ubunge wake kisa Makonda

Mch. Peter Msigwa, Mbunge wa Iringa Mjini
Spread the love

MBUNGE wa Iringa Mjini, Mchungaji Peter Msigwa amesema yupo tayari kujiuzuru ubunge wake kama itathibitika kuwa amemtelekeza mtoto kwa mwanamke mmoja jijini Dar es Salaam. Anaripoti Mwanadishi Wetu … (endelea).

Mch. Msigwa ametajwa na mwanamke mmoja kati ya walioripoti katika ofisi za Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda kuwa ametelekeza mtoto.

Makonda ametoa nafasi kwa wanawake waliotelekezwa na wanaume waliowazalisha, ndipo mwanamke huyo ambaye hajatajwa jina lake alifika katika ofisi za Mkuu wa Mkoa na kueleza kuwa amezalishwa na mbunge huyo na kumtelekeza bila matunzo yoyote.

Katika taarifa yake, Mch. Msigwa amesema kinachoelezwa kuwa ametelekeza mtoto jijini na mwanamke huyo ni propaganda za makusudi zenye lengo la kujaribu kumchafua.

Msigwa amesema: “Kama huyo mama ambaye jina lake limehifadhiwa yupo, nataka ajitokeze pamoja na mtoto niliyemtelekeza. Kwa sasa nipo Dodoma Bungeni; anaweza kunipata kupitia Spika wa Bunge au Katibu wa Bunge au Kiongozi wa Upinzani Bungeni.”

Mbunge huyo amesema kama ikithibitika kuna mtoto amemtelekeza yupo tayari kujiuzuru Ubunge.

 

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mpwa wa Magufuli mbaroni kwa kusambaza picha za utupu

Spread the loveJESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata...

error: Content is protected !!