Tuesday , 5 December 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Mbunge ashangaa Ranchi ya NARCO kubadilishwa matumizi
Habari za Siasa

Mbunge ashangaa Ranchi ya NARCO kubadilishwa matumizi

Sophia Mwakagenda
Spread the love

SERIKALI imetakiwa ieleze, kwanini Ranchi ya NARCO Mbarali iliyoanzishwa kwa ajili ya mifugo, imeacha matumizi yake na sasa eneo hilo linatumika kwa kilimo? Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma … (endelea).

Swali hilo limeulizwa na Sophia Mwakagenda, Mbunge wa Viti Maalum (Chadema) leo tarehe 14 Aprili 2020, jijini Dodoma wakati wa kipindi cha maswali majibu.

Wizara ya Mifugo ikijibu swali hilo imeeleza, Ranchi ya Usangu iliyopo wilayani Mbarali ni miongoni mwa ranchi ambazo serikali ilielekeza zigawanywe katika vitalu na kukodishwa kwa wawekezaji, ili kuendeleza ufugaji wa kisasa na kibiashara kwa mikataba maalum.

Wizara imesema, katika mpango huo, Ranchi hii iligawanywa katika vitalu 16 vyenye ukubwa wa kati ya hekta 2,448.90 hadi 3,158.88 na kukodishwa kwa wawekezaji wazawa. Kwa sasa Ranchi hiyo ina jumla ya ng’ombe 9,885, mbuzi/kondoo 6,192, punda 56 na farasi wawili (2).

“NARCO imekwishafanya tathmini na kubaini jumla ya wawekezaji katika vitalu vitano ambao wamekiuka masharti ya uwekezaji kwa kutumia mashamba hayo kwa shughuli za kilimo.

“Hivyo NARCO imechukua hatua za kisheria, ikiwemo kutoa notisi za kuonesha nia ya kuvunja mikataba na kuwaondoa wawekezaji hao na maeneo yao yatakodishwa kwa wafugaji wengine wenye nia ya kuwekeza kwa mujibu wa sheria,” wizara imeeleza na kuongez:

“Ili kupunguza migogoro ya wakulima na wafugaji, NARCO kwa sasa inaendelea na zoezi la kuweka mipaka inayoonekana katika Ranchi zake zote ikiwemo Ranchi ya Usangu.”

Wizara imeeleza kuwa, imeanzisha mpango wa kuwakodisha wafugaji maeneo kwa muda mfupi kwa utaratibu wa mikataba maalum.

“Katika mwaka 2019/2020, jumla ya vitalu 107 vimekodishwa kwa wafugaji katika Ranchi zake zote. Aidha kwa kushirikiana na Ofisi ya Mkuu wa Wilaya Mbarali, NARCO imeanza zoezi la kuwabaini wafugaji walio tayari kuwekeza katika maeneo ambayo wataondolewa wawekezaji waliokiuka masharti ya mkataba,” imeeleza wizara.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Dk. Biteko: Viongozi tuache alama nzuri katika utendaji wetu

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

Habari za SiasaTangulizi

Chanzo maporomoko yaliyoua 65 Hanang, chatajwa

Spread the loveSERIKALI imesema kumeguka kwa sehemu ya Mlima Hanang ambao ilikuwa...

Habari za Siasa

Baba yake Ole Sabaya ashinda Uenyekiti CCM – Arusha

Spread the loveLoy Thomas Sabaya ambaye ni Baba wa aliyekuwa Mkuu wa...

Habari za Siasa

Serikali yaagiza uchunguzi chanzo maporomoko Hanang

Spread the loveSERIKALI imeagiza uchunguzi ufanyike ili kubaini chanzo cha maporomoko ya...

error: Content is protected !!