Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mbunge aliyefariki alizuiwa kupanda ndege kwenda Dar
Habari za SiasaTangulizi

Mbunge aliyefariki alizuiwa kupanda ndege kwenda Dar

Spread the love

MWENYEKITI wa Kamati ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira, David Kihenzile amesema siku moja kabla ya Mbunge Irene Ndyamkama kufikwa na umauti, alizuiwa kusafiri kwa ndege kuelekea mkoani Dar es Salaam kwa ajili ya kukagua viwanda. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea)

Amesema Irene ambaye alikuwa mjumbe wa kamati hiyo ya Bunge, baada ya kuzuiwa kusafiri kwa ndege alisafiri kwa gari.

Kihenzile ametoa kauli hiyo leo Jumatano tarehe 27 Aprili, 2022 wakati akitoa salamu kwa niaba ya kamati ya Viwanda ambayo marehemu Iren alikuwa mjumbe.

“Jumamosi tarehe 23, Aprili 2022 tulikuwa tunakwenda Dar es Salaam kutembelea viwanda, pamoja na hali yake aliyokuwa nayo alisema lazima ‘niende nikashiriki’. Hata hivyo tulipofika Airport Dodoma hakuweza kuendelea kutokana na logistics za hapa na pale.

“Lakini bado akasema mimi nitakwenda hata kwa gari hivyo sisi tukatangulia lakini akiwa pale alisalimia wajumbe wote wa kamati akiwa na furaha na matumaini makubwa kwamba ataungana na wenzake kukagua viwanda mbalimbali Dar es Salaam,” amesema.

Ameongeza kuwa wao (wajumbe) waliondoka Dodoma kwa ndege na walipofika Dar es Salaam, Irene alichelewa kutokana na changamoto alizozipata njia.

“Kesho yake wakati tunajiandaa kurudi tukapata taarifa kwamba mwenzetu ametanguliwa mbele za haki kwa kweli ilitusikitisha sana,” amesema.

… ALIKUWA MJAMZITO

Aidha, Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake wa CCM (UWT), Gaudensia Kabaka amesema Irene alikuwa ni mjamzito na kwamba kuna mambo mengi aliyokuwa ameyapanga kuyafanya baada ya kujifungua.

Kabaka ameeleza kuwa baada ya kutembelea ofisi za UWT aliahidi kukamilisha ujenzi wa nyumba ya Katibu bwa UWT mkoa wa Rukwa baada ya kujifungua.

“Alinitembelea na kutueleza mipango yake kwa wanawake, jinsi anavyotaka kuwafanyia wanawake wa Rukwa.

“Alitueleza ameanza kujenga nyumba ya Katibu wa umoja huo mkoa wa Rukwa… na baada ya kujifungua katika uzinduzi mmoja wetu atawenda kuifanya hiyo kazi lakini imempendeza Mungu kwamba Irene hajafikia azma hiyo,” amesema.

Ndyamkama alifariki tarehe 24 Aprili, 2022 katika hospitali ya Tumbi Kibaha alikokwenda kupatiwa matibabu baada ya kuugua akiwa safari kutoka Dodoma kuelekea Dar es Salaam na ameacha mume na watoto watatu.

1 Comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!