Thursday , 2 May 2024
Home Kitengo Biashara Mbunge aibana Serikaili utitiri mashauri ya kikodi
Biashara

Mbunge aibana Serikaili utitiri mashauri ya kikodi

Spread the love

MBUNGE Viti Maalum, Janejelly Ntate, amehoji mkakati wa Serikali katika kumaliza mashtaka ya kikodi yaliyoko kwenye bodi ya rufani za kodi na baraza la rufani za kodi, ili matrilioni ya fedha zinazozibishaniwa zirudi serikalini kwa ajili ya kuhudumia wananchi. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam…(endelea).

Ntate amehoji hayo leo tarehe 10 Novemba 2023, bungeni jijini Dodoma, katika kipindi cha maswali na majibu.

Akijibu swali hilo, Waziri wa Fedha, Dk. Mwigulu Nchemba, Serikali inaendelea kutekeleza mpango maalum kuanzia Novemba 2023 hadi Juni 2024, wenye lengo la kumaliza mashauri ya kikodi yaliyofunguliwa. Pia, imeunda taasisi ya msuluhishi wa malalamiko ya kikodi kwa ajili ya kupokea na kuyatatua.

Waziri huyo wa fedha amesema, amesema hadi kufikia Oktoba 2023, bodi ya rufani za kodi ilikuwa na mashauri 889 yenye kiasi cha kodi kinachobishaniwa cha Sh. 6.46 trilioni na Dola za Marekani 4.66 milioni.

Amesema bodi imeshasikiliza mashauri 167 kati ya 889 ambayo yenye thamani ya Sh. 2.66 trilioni na Dola 210,000.

Kwa upande wa Baraza la Rufani za Kodi, Dk. Mwigulu amesema kuna mashauri 176 yenye kiasi cha kodi kinachobishaniwa kiasi cha Sh. 266.94 bilioni, ambapo mashauri 91 yenye kodi Sh. 166.3 bilioni, yamesikilizwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Biashara

Cheza sloti ya Zombie Apocalypse na ushinde kirahisi

Spread the love Wengi wetu hupenda filamu za Mazombie huwa zinatishakidogo lakini...

Biashara

Ushirikishwaji wa wafanyakazi ni muhimu katika utekelezaji wa sera za afya na usalama kazini

Spread the love  KILA ifikapo Aprili 28 ya kila mwaka, dunia huadhimisha...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Oryx gesi yagawa mitungi, majiko 100 kwa waandishi wa habari Dar

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gesi Tanzania imegawa mitungi 100 ya gesi...

Biashara

Wazir Jr kinara wa ufungaji KMC FC ajiunga Meridianbet

Spread the love    MUITE Wazir Jr ‘The King of CCM Kirumba’,...

error: Content is protected !!