Sunday , 28 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mbowe: Mwinyi chanzo cha mageuzi
Habari za SiasaTangulizi

Mbowe: Mwinyi chanzo cha mageuzi

Spread the love

MWENYEKITI wa Chama cha Demokrasia, Freeman Mbowe amesema huwezi kuliacha jina la Ally Hassan Mwinyi unapotaja mageuzi nchini. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Kupitia ukurasa wake wa mtandao wa X, Mbowe amesema wakati Mzee Mwinyi anaingia madarakani kama Rais wa awamu ya Pili mwaka 1985, alipokea nchi ambayo ilikua na changamoto lukuki.

“Tanzania kwa kipindi kile ilikua katika harakati za kutafuta namna bora zaidi ya kusonga mbele baada ya kipindi cha ujamaa.

“Miaka ya urais wake iliyompa jina la utani la Mzee Rukhsa ilikua msingi wa ujenzi wa taifa lenye dira na muelekeo mpya.  Rais Mwinyi atakumbukwa sio tu kwa vyeo na uraisi bali pia uwajibikaji, na ubinadamu wake.

“Taifa limepoteza kisima cha busara na nembo muhimu. Natoa pole zangu dhati kwa familia, ndugu, jamaa na taifa kwa msiba huu mzito.  Inna lillahi wa inna ilayhi raji’un,” ameandika Mbowe.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Sauti ya Watanzania waeleza sababu za kuiunga mkono Chadema

Spread the love  KIKUNDI kinachojipambanua katika kupigania rasilimali na uhuru wa nchi,...

Habari MchanganyikoTangulizi

Jacob, Malisa waachiwa kwa masharti

Spread the love  JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

error: Content is protected !!