Wednesday , 8 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mbowe alaani ukamatwaji wa Lissu, “Tuna hofu kubwa”
Habari za SiasaTangulizi

Mbowe alaani ukamatwaji wa Lissu, “Tuna hofu kubwa”

Freeman Mbowe, Mwenyekiti wa Chadema
Spread the love

MWENYEKITI wa Chadema, Freema Mbowe amelaa ukamataji, unyanyasaji, usumbufu aliodai unafanywa  na Jeshi la Polisi na vyombo vingine vya Dola kwa Makamu Mwenyekiti wa Chama hicho, Tundu Lissu. Anaripoti Mwandishi Wetu …(endelea).

Kwa mujibu wa taarifa aliyoweka kwenye ukurasa wake wa Twitter, Mbowe amesema Chadema kinalaani ukamati huo pia kwa viongozi wengine waandamizi wa ngazi mbalimbali, wanachama na wapenzi wa chama hicho mkoani Arusha.

“Kwa uzito huo huo, tunalaani uzuiaji wa mikutano yetu na shughuli halali za kisiasa huko Ngorongoro, Loliondo na Karatu.

“Tuna hofu kubwa ya usalama wa watu wetu na ni dhahiri sasa Serikali ya Rais Samia Suluhu Hassan inarejesha utawala wa mabavu usiothamini haki, Uhuru na Demokrasia. Tunafuatilia kwa karibu na tunadai kuachiliwa haraka na bila masharti kwa watu wetu wote!,” ameandika Mbowe.

Taarifa hiyo ya Mbowe imekuja saa chache baada ya Jeshi la Polisi mkoani Arusha kukiri kumkamata Lissu na wenzie watatu kwa ajili ya mahojiano kuhusu tuhuma za kufanyq mikusanyiko isivyo halali na kuzuia Polisi kutekeleza majukumu yake.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Rais Samia ni Mzanzibari: Shida Iko Wapi?

Spread the loveTAIFA linakabiliwa na upungufu wa fikra sahihi. Upungufu huu unaonekana...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Mpina mwiba CCM, ahofia kuzibwa mdomo

Spread the loveWAKATI Chama cha Mapinduzi (CCM), kikijinasibu kuwa kinara wa demokrasia...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Mabeyo ametuepusha

Spread the loveNIMEGUSWA na uadilifu, utiifu na uaminifu wa Mkuu mstaafu wa...

Habari za SiasaTangulizi

CCM yaitaka TAKUKURU kuichunguza Chadema tuhuma alizoibua Lissu

Spread the loveCHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimeitaka Taasisi ya Kuzuia na Kupambana...

error: Content is protected !!