Friday , 3 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Marekani kuwafunda wanasiasa uwajibikaji na uwazi, ACT-Wazalendo kunufaika
Habari za Siasa

Marekani kuwafunda wanasiasa uwajibikaji na uwazi, ACT-Wazalendo kunufaika

Spread the love

KATIBU MKuu wa Chama cha ACT-Wazalendo, Ado Shaibu, anatarajiwa kushiki mafunzo kuhusu masuala ya uwazi na uwajibikaji, yaliyoandaliwa na Serikali ya Marekani kupitia mpango wa Program ya Uongozi ya International Visitor Leadership Program (IVLP). Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam…(endelea).

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Katibu wa Idara ya Mambo ya Nje, ACT-Wazalendo, Mwanaisha Mndeme, mafunzo hayo yanafanyika kuanzia tarehe 8 hadi 26 Aprili 2024, nchini Marekani.

“Dhima ya program ya IVLP ya 2024 inayoratibiwa na Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani ni uwazi na uwajibikaji wa taasisi za umma. Ado atajumuika na washiriki wengine ambao ni viongozi kutoka taasisi zinazohusika na masuala ya uwazi na uwajibikaji kutoka nchi 24,” imesema taarifa ya Mndeme na kuongeza:

“Kwenye program hiyo, kwa kipindi cha wiki tatu, Ado na washiriki wengine watapata nafasi ya kupata uzoefu wa jinsi taasisi za Marekani zinazohusika na masuala ya uwazi na uwajibikaji zinavyofanya kazi.”

Chama cha ACT-Wazalendo ni miongoni mwa vyama vya siasa vya upinzani nchini Tanzania, vinavyosimamia masuala ya uwazi na uwajibikaji serikalini kupitia njia mbalimbali, ikiwemo uchambuzi wa ripoti za Mdhibiti na Mkaguzi wa Mahesabu ya Serikali (CAG) zinazotolewa kila mwaka, lengo ni kuonyesha maeneo yenye dosari na kisha kutoa mapendekezo juu ya namna ya kuboresha.

Pia, ACT-Wazalendo kimeunda Baraza Kivuli la Mawaziri linalosimamia utendaji wa Serikali wa kila siku, baada ya wapinzani kukosa uwakilishi wa kutosha bungeni.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Sabaya afutiwa kesi, ruksa kugombea uongozi

Spread the loveMwendesha Mashtaka Mkuu wa Serikali DPP leo Ijumaa amefuta rufaa...

Habari za Siasa

Serikali yasaka bilioni 3 kujenga daraja Mto Mpiji

Spread the loveSerikali imesema inaendelea na juhudi za kutafuta fedha kiasi cha...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kwafukuta kisa chaguzi, Lissu aibua tuhuma nzito

Spread the loveCHAGUZI za kusaka viongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

error: Content is protected !!