Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Makonda awapopoa wanaomtofautisha Magufuli na Samia
Habari za SiasaTangulizi

Makonda awapopoa wanaomtofautisha Magufuli na Samia

Spread the love

KATIBU wa Itikadi na Uenezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Paul Makonda, amewataka viongozi wa chama hicho na watu wanaojaribu kumtenganisha Rais Dk. Samia Suluhu Hassan na Hayati Dk. John Magufuli, waache mara moja. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam…(endelea).

Akizungumza katika hafla ya kupokea ndege mpya ya Kampuni ya Ndege ya Tanzania (ATCL), leo Jumatatu jijini Dar es Salaam, Makonda amedai kuna viongozi uchwara ambao wanajipendekeza kwa Rais Samia ili kumfanya kama sio sehemu ya Magufuli.

“Kuna kasumba ya ujinga unaoendelea wa kutaka kumtofautisha Dk. Samia na Dk. Magufuli, huwezi kuwatenganisha hao watu na viongozi wengi wanafiki wanaotafuta kujipendekeza kwa Dk. Samia, kila wakipata jukwaa wanataka kumfanya kama Dk. Samia si sehemu ya Dk. Magufuli. Kama msemaji wa chama tukazunguka na ilani ya chama chetu anachokifanya Dk. Samia ndicho ambacho alikifanya Dk. Magufuli,” amesema Makonda.

Makonda amesema “na walisimama wakazunguka katika taifa hili wakatafuta kura kwa pamoja, huwezi ukawatenganisha na waziri mkuu wao yule pale, Kassim Majaliwa, ningetamani leo iwe ndiyo siku ya mwisho ya unafiki wa viongozi na wanasiasa uchwara wanaopambana kuwatenganisha viongozi hawa.”

Makonda alitoa kauli hiyo akizungumzia mafanikio ya miaka mitatu ya Rais Samia madarakani, aliyepewa mamlaka Machi 19, 2021 baada ya Magufuli kufariki dunia akiwa madarakani. Tangu alivyoingia madarakani Rais Samia amekuwa akiendeleza miradi iliyoachwa na mtangulizi wake, ikiwemo ununuzi wa ndege kwa ajili ya kuimarisha ATCL.

“Mafanikio haya tunayesherehekea wote kwa sababu chama ni kimoja, serikali ni ya CCM na nyie wananchi mliipigia kura,” amesema Makonda.

Kauli ya Mikonda imekuja siku kadhaa tangu Rais Samia kuweka bayana kwamba yeye hana makundi na kwamba yeye anafanya kazi na makundi yote. Alitoa kauli hiyo wakati akitaja sababu za kufanya mabadiliko ya wakuu wa mikoa na wilaya, aliyoyafanya hivi karibuni.

“Mwanzo niliwaambia mlitarajia nitawateua kwa makundi, lakini mimi Samia sina kundi, mkijitazama hum ohayo makundi mnayojua makundi yenu nyote mpo humo ndani, ninachotaka mimi watanzania kwa pamoja tufanye kazi tusogeze nchi yetu mbele, sina kundi sasa wale wanaosema huyu ni wa mama huyu sio wa mama, mimi mama nina watoto wote,” alisema Rais Samia.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za SiasaTangulizi

Samia awataka watanzania kudumisha muungano

Spread the loveRais wa Tanzania,Samia Suluhu Hassan amewataka Watanzania kuendeleza Muungano kwa...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

error: Content is protected !!