Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Tangulizi Majaliwa: Mikoa, wilaya mpya hadi sensa ifanyike
Tangulizi

Majaliwa: Mikoa, wilaya mpya hadi sensa ifanyike

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa
Spread the love

WAZIRI Mkuu wa Tanzania, Kassim Majaliwa amesema Serikali imesitisha utaratibu wa kugawa mikoa, wilaya, kata, vijiji vipya hadi hapo sensa itakapofanyika mwaka 2022. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea)

Majaliwa ametoa kauli hiyo leo tarehe 9 Septemba bungeni jijini Dodoma wakati akijibu swali la Mbunge wa viti maalumu, Aleksia Kamguna (CCM).

Mbunge huyo alihoji ni lini mikoa ya Tabora, Tanga na Morogoro itagawanya kwa kuwa ni mikoa mikubwa hali iliyosababisha huduma za kijamii kama vile afya kudorora.

Akijibu swali hilo Majaliwa alikiri kuwa ni kweli mikoa hiyo ni mikubwa sana ikilinganishwa na mikoa mingine na taarifa kwa maandishi imekwishawasilishwa serikalini.

“Serikali tulisitisha kutoa maeneo mapya ya utawala kutaka kuimarisha maeneo mapya ambayo ni vijiji, kata, wilaya na mikoa ili kuwe na miundombinu ya kutosha na watumishi.

“Pia tumesitishaili tunasubiri sensa ya mwaka 2022 ili kupata takwimu halisi ya idadi ya wakazi itakayoturahisisha kufanya uamuzi kulingana na ukubwa wa eneo kwa kuzingatia vigezo tunavyotumia. Baada ya sensa itafanya maamuzi,” amesema.

1 Comment

  • Taarifa hii ni tamu mno. Tunaisubiri kwa hamu hiyo sensa.

    Asante sana kwa kuandaa sensa hiyo. Ninaamini itatusaidia sana kufanya maamuzi fulani fulani kwa ajili ya maendeleo yetu na taifa kwa ujumla.

    Rafiki yako,

    Aliko Musa.

    Real estate investment consultant

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari za SiasaTangulizi

Mpwa wa Magufuli mbaroni kwa kusambaza picha za utupu

Spread the loveJESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata...

Habari za SiasaTangulizi

Shibuda amlima waraka mzito Bulembo

Spread the loveMKONGWE wa siasa nchini, John Shibuda amemshukia kada maarufu wa...

Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia ataja mikakati ya kufikia trilioni 2 biashara Uturuki, Tz

Spread the loveWakati Tanzania na Uturuki zikidhamiria kuongeza kiwango cha biashara hadi...

error: Content is protected !!