Friday , 3 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Majaliwa awataka wananchi kuitumia kampeni ya Samia Aid kutokomeza ukatili
Habari Mchanganyiko

Majaliwa awataka wananchi kuitumia kampeni ya Samia Aid kutokomeza ukatili

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa
Spread the love

 

WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amewataka wananchi watumie huduma ya msaada wa kisheria ya Mama Samia (Samia Legal Aid Campaign), kutokomeza vitendo vya ukatili wa kijinsia. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Majaliwa ametoa wito huo jana Alhamisi, akizindua kampeni hiyo kwa mkoa wa Dodoma, inayoanza leo tarehe 28 Aprili 2023, katika halmashauri nane mkoani humo ikiwemo Mpwapwa, Kondoa, Bahi na Dodoma Mjini.

“Kampeni hii itasadia kuboresha upatikanaji wa haki kwa watu wasiojiweza, hususan wanawake, watoto na makundi mengine yaliyo katika mazingira magumu. Vilevile itachangia kuimarisha amani na utulivu, kuongeza kipato na kuleta utengamano wa kitaifa,” amesema Waziri Majaliwa.

Majaliwa amesema kampeni hiyo itasadia kuimarisha mfumo wa utoaji Huduma za msaada wa kisheria kuanzia Serikali kuu hadi Serikali za Mitaa.

Aidha, Majaliwa ameiagiza Wizara ya Katiba na Sheria, iweke mfumo mzuri wa kushighulikia changamoto za kisheria zitakazoibuliwa wakati wa kampeni hiyo.

Katika kampeni hiyo, kata 80 na vijiji 240, vinatarajiwa kufikiwa na kampeni hiyo, iliyozinduliwa kitaifa tarehe 15 Februari mwaka huu.
Kampeni hiyo inayotekelezaa chini ya Wizara ya Katiba na Sheria kwa kushirikiana na Shirika la Legal Services Facility (LSF) na mashirika mengine, imepewa jina la Samia, ili kuenzi mchango wa Rais Samia Suluhu Hassan, katika kutokomeza vitendo vya ukatili hasa kwa kina mama, watoto na makundi Maalum.

Kampeni hiyo inafanyika kwa miaka mitatu mfululizo, kuanzia Machi 2023 Hadi Desemba 2025.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB yang’ara maonesho OSHA

Spread the loveBenki ya NMB imebeba tuzo ya kampuni bora kwenye sekta...

Habari MchanganyikoKimataifa

Ruto amteua Kahariri kuwa mkuu wa majeshi

Spread the loveRAIS wa Kenya, William Ruto, amemteua Jenerali Charles Muriu Kahariri,...

Habari Mchanganyiko

Chongolo aonya viongozi vijiji kutouza NIDA kwa wageni

Spread the loveMKUU wa Mkoa wa Songwe, Daniel Chongolo amewaonya viongozi wa...

error: Content is protected !!