Thursday , 2 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Majaliwa avutiwa na mchango wa NBC kuchochea kasi ya kilimo, biashara na michezo
Habari Mchanganyiko

Majaliwa avutiwa na mchango wa NBC kuchochea kasi ya kilimo, biashara na michezo

Spread the love

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ameonyesha kuvutiwa na mchango unaoendelea kutolewa na benki ya Taifa ya Biashara (NBC) katika kukuza sekta mbalimbali nchini ikiwemo kilimo, biashara na michezo kupitia huduma na ufadhili wa benki hiyo kwenye maeneo hayo. Anaripoti Mwandishi Wetu …(endelea).

Waziri Mkuu Majaliwa alitoa pongezi hizo alipotembelea banda la benki hiyo lililopo kwenye viunga vya ukumbi wa Mkutano Mkuu wa saba  wa mwaka wa Jukwa la Wahariri Tanzania (TEF), unaofanyika Mkoani Lindi. Benki ya NBC ni moja ya wadhamini muhimu wa Mkutano huo wa siku mbili.

Akiwa kwenye banda hilo Waziri Mkuu alipata wasaa wa kupata maelezo kuhusu huduma mbalimbali zinazotolewa na benki hiyo katika sekta mbalimbali ambapo alionyesha kuvutiwa na huduma ya NBC Shambani inayotolewa na benki hiyo mahususi kwa wakulima wakiwemo wakulima wa zao la korosho.

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa (kulia) akitazama baadhi ya vipeperushi kuhusu huduma  zinazotolewa na Benki ya NBC huku akimsikiliza Meneja wa NBC tawi la Lindi, Iovin Mapunda (Kushoto) akitoa maelezo kuhusu huduma mbalimbali zinazotolewa na benki hiyo ikiwemo akaunti ya NBC Shambani mahususi kwa wakulima wakati Waziri mkuu alipotembelea banda la benki hiyo lililopo kwenye viunga vya ukumbi wa Mkutano Mkuu wa saba  wa mwaka wa Jukwa la Wahariri Tanzania (TEF), unaofanyika Mkoani Lindi. Benki ya NBC ni moja ya wadhamini muhimu wa Mkutano huo wa siku mbili.

Waziri Mkuu Majaliwa pia aliipongeza benki hiyo kwa mchango wake kwenye sekta ya michezo hususani udhamini wake kwenye Ligi Kuu ya Tanzania Bara yaani NBC Premiere League, Ligi ya Vijana pamoja na NBC Championship.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

NEMC yatoa elimu matumizi sahihi ya zebaki kwa wachimbaji

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC)...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Oryx gesi yagawa mitungi, majiko 100 kwa waandishi wa habari Dar

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gesi Tanzania imegawa mitungi 100 ya gesi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari MchanganyikoMichezo

Wanamichezo Mei Mosi wachangia wahitaji vitu vya mil. 11.5

Spread the loveWanamichezo wanaoshiriki Michezo ya Mei Mosi Taifa 2024 jijini Arusha...

error: Content is protected !!