Thursday , 2 May 2024
Home Kitengo Biashara Majaliwa afungua kongamano la nishati, atembelea banda la NMB
Biashara

Majaliwa afungua kongamano la nishati, atembelea banda la NMB

Spread the love

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amesema Tanzania haitegemei kuzalisha umeme kwa kutumia maji pekee bali inaendelea kuweka mkazo katika uzalishaji wa umeme kwa kutumia nishati nyingine kama gesi na jua ili kuwa mzalishaji mkubwa na nishati hiyo. Anaripoti  Mwandishi Wetu…(endelea)

Majaliwa ametoa kauli hiyo leo tarehe 20 Septemba 2023 wakati akifungua Kongamano la Tano na Maonesho ya Nishati Tanzania na kupata maelezo kuhusu utayari wa Benki ya NMB kuwekeza kwenye maendeleo ya nishati.

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa (kushoto) akipata maelezo kutoka kwa Meneja Mwandamizi Idara ya Wateja Wakubwa upande wa Nishati wa Benki ya NMB, Hamis Njapuka, kuhusu utayari wa Benki ya NMB kwenye suala zima la maendeleo ya nishati, wakati wa kongamano la kimataifa la Nishati “Tanzania Energy Congress” lililofanyika jijini Dar es Salaam jana na kudhaminiwa na Benki ya NMB.

Majaliwa baada ya kufungua kongamano hilo la siku mbili linalofanyika katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Julius Nyerere, Dar es Salaam, ametembelea banda la Benki ya NMB na kupata maelezo kutoka kwa Meneja Mwandamizi Idara ya Wateja Wakubwa upande wa Nishati wa NMB, Hamis Njapuka, kuhusu utayari wa benki hiyo kuwekeza kwenye maendeleo ya nishati.

“Tunaendelea na utafutaji wa gesi, tunataka tuwe wazalishaji wakubwa wa nishati, tuwe na umeme wa kutosha utakaopatikana kwa urahisi na nafuu na ziada tutauza nje ya nchi,” amesema Majaliwa.

Waziri Mkuu amesema katika kongamano hilo la kimataifa la nishati ambalo limehusisha  viongozi na wadau kutoka katika mataifa mbalimbali duniani litajadili namna bora ya kukabiliana na changamoto ya upatikanaji wa nishati.

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa (kushoto) akizungumza na Meneja Mwandamizi Idara ya Wateja Wakubwa upande wa Nishati wa Benki ya NMB, Hamis Njapuka, wakati wa kongamano la Kimataifa la Nishati “Tanzania Energy Congress” lililofanyika jijini Dar es Salaam jana na kudhaminiwa na Benki ya NMB.

Kwa upande wake, Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko amesema wameendelea kutekeleza mipango mbalimbali waliojiwekea katika kuhakikisha umeme unapatikana wakati wote nchini.

Dk. Biteko amesema zaidi ya kampuni 100 za nishati kutoka katika maeneo mbalimbali duniani zinashiriki katika kongamano hilo ambalo lilitanguliwa na mkutano wa viongozi wa nishati.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Biashara

Cheza sloti ya Zombie Apocalypse na ushinde kirahisi

Spread the love Wengi wetu hupenda filamu za Mazombie huwa zinatishakidogo lakini...

Biashara

Ushirikishwaji wa wafanyakazi ni muhimu katika utekelezaji wa sera za afya na usalama kazini

Spread the love  KILA ifikapo Aprili 28 ya kila mwaka, dunia huadhimisha...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Oryx gesi yagawa mitungi, majiko 100 kwa waandishi wa habari Dar

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gesi Tanzania imegawa mitungi 100 ya gesi...

Biashara

Wazir Jr kinara wa ufungaji KMC FC ajiunga Meridianbet

Spread the love    MUITE Wazir Jr ‘The King of CCM Kirumba’,...

error: Content is protected !!