Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Madiwani wawachongea wezi wa mapato ya mazao
Habari za Siasa

Madiwani wawachongea wezi wa mapato ya mazao

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Chamwino, Athumani Masasi
Spread the love

MADIWANI wa Halmashauri ya wilaya ya Chamwino, Dodoma wamemuomba  Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri hiyo, Athumani Masasi, kuwachukulia hatua za kinidhamu watumishi wanaoibia mapato ya ushuru wa mazao waliopo kwenye vizuizi vilivyopo vijijini. Anaripoti Danson Kaijage, Chamwino … (endelea).

Kauli hiyo imetolewa kwa pamoja na madiwani hao wakati walipokuwa wakichangia kwenye kikao cha baraza la madiwani cha kujadili taarifa za utekeleaji za kamati za kudumu zilizotolewa na wenyeviti kilichofanyika Chamwino.

Akizungumza kwa niaba ya madiwani wengine Mwenyekiti wa Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango,  Samwel Kaweya alisema kuwa baadhi ya watumishi waliopewa dhamana ya kukusanya ushuru wa mazao siyo waaminifu na hawana uchungu wa halmashauri hiyo.

“Hivyo tunakuomba Mkurugenzi wetu kuwa macho kwa watumishi hao  wanaofanya kazi kwenye vizuizi ambao walipewa dhamana ya kukusanya ushuru,baadhi yao siyo waaminifu kwa upande wa fedha pia wanatuangusha hawa,” alisema.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Chamwino, Athumani Masasi amewataka watumishi wake kusimamia kwa uaminifu na ueledi katika ukusanyaji wa  vyanzo vya mapato kwa vitendo. Ili kuiongezea halmashauri mapato ya kutosha.

Alisema ili kuvuka  malengo ya ukusanyaji wa mapato hayo watendaji waliopewa dhamana wakasimamia kwa uaminifu vyanzo vyote vinavyoiingizia halmashauri mapato ikiwa kwenye ushuru wa mazao.

“Madiwani na watendaji inatubidi kuongeza kasi katika ukusanyaji wote wa vyanzo vya mapato, li tuweze kufikia malengo ya juu zaidi, hii inawezekana pale ambapo kila mtumishi atasimama kwenye sehemu yake kwa uaminifu pia watakuwa wakimuunga mkono juhudi zake Rais John Magufuli katika mpango wake uchumi wa viwanda vya kati,” alisema.

Katika kikao hicho kamati mbalimbali zilipitisha bajeti zake za robo mwaka wa pili ya 2018/19 Oktoba hadi Desemba ikiwemo ya fedha na mipango, ambayo ilikusanya jumla ya Sh. 16,705,663,412 kutoka kwenye vyanzo vyake vya mapato ambayo ni sawa na asilimia 43 ya makisio ya mwaka wa fedha.

Huku kamati zingine zikichangia mamilioni ya fedha kwa ajili ya utekelezaji wa shughuli mbalimbali za miradi ya maendeleo kwa ajili ya Halmashauri hiyo ya Chamwino.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!