Friday , 2 June 2023
Home Kitengo Habari Kimataifa Rais wa Nigeria ashitakiwa mahakamani
Kimataifa

Rais wa Nigeria ashitakiwa mahakamani

Goodluck Jonathan, Rais Mstaafu wa Nigeria
Spread the love

SERIKALI ya Nigeria imemshitaki aliyekuwa Rais wa Taifa hilo, Goodluck Jonathan katika Mahakama ya Biashara ya London, kwa tuhuma za kupokea rushwa kutoka kwa kampuni ya Mafuta ya Anglo-Dutch Shell na Italian Peer Eni. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa … (endelea).

Katika kesi hiyo, Serikali ya Nigeria inamtuhumu Rais Mstaafu, Jonathan pamoja na aliyekuwa Waziri wa Mafuta wakati wa utawala wake, Diezan Alison-Madueke, kuvunja sheria za nchi hiyo na kuikosesha mapato.

Serikali ya Nigeria inadai kuwa, Rais Jonathan pamoja na Madueke walitoa haki ya uchimbaji mafuta kwa kampuni ya Mafuta ya Anglo-Dutch Shell na Italian Peer Eni, na kwamba thamani ya mafuta inayoonekana katika mkataba huo ni tofauti na thamani halisi ya mafuta yaliyopo katika eneo la uchimbaji.

Mahakama hiyo imeelezwa  na Serikali ya Nigeria kuwa, thamani ya mafuta ni zaidi ya dola 3.5 bilioni kiasi ambacho ni tofauti na inavyo onekana kwenye mkataba wa nchi hiyo na Kampuni za Mafuta ya Anglo-Dutch Shell na Italian Peer Eni, ambao unaonesha thamani yake kuwa ni dola 209 milioni.

Pia, Tume ya Uchumi na Fedha nchini Nigeria imesema inajiandaa kuwafungulia mashataka viongozi wengine wa zamani waliohusika na sakata hilo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Kimataifa

Kauli ya Rais wa China kuhusu ajira yawakatisha tamaa vijana

Spread the love  KAULI ya hivi karibuni ya Rais wa China, Xi...

KimataifaMakala & Uchambuzi

Jeshi la Sudan lasitisha mazungumzo na wanamgambo wa RSF

Spread the love  JESHI rasmi la serikali ya Sudan, limesitisha ushiriki wake...

Kimataifa

Wakimbizi laki mbili wa Kongo, Burundi kuhemea chakula

Spread the love  SHIRIKA la Chakula la Umoja wa Mataifa (WFP), limetangaza...

Kimataifa

Mkutano wa Quad Hiroshima waibuka na kutafuta amani na ustawi wa Indo-Pacific

Spread the love  JITIHADA za mazungumzo ya Pande Nne (Quad), hazikuthaminiwa na...

error: Content is protected !!