MAKAMU wa Rais Tanzania, Samia Suluhu Hassani amewaonya tabia ya madiwani kutumia fedha za mifuko ya kuwezesha wananchi kwa ajili ya masilahi yao binafsi ya kisiasa. Anaripoti Mwandishi Wetu, Tanga … (endelea).
Mama Samia metoa kauli hiyo leo Jumatano, tarehe 17 Machi 2021, katika viwanja vya Tangamano, Tanga Mjini, ikiwa ni siku ya tatu kati ya tano ya ziara yake mkoani humo.
Amesema, diwani yeyote atakayebainika kutumia vibaya fedha hizo, atachukuliwa hatua.
“Wito wangu, mfuko huu sasa usitumike kama mfuko wa kisiasa kwa madiwani.”
“Ndugu zangu madiwani, mfuko huu mlikuwa mmeugeuza kujijenga kisiasa. kila mtu anavutia kwake, tumewafumbia macho kipindi hiki, kipindi kijacho nasimama na nyie,” amesema Mama Samia.
Ametoa onyo hilo baada ya kubaini upotevu wa fedha za mifuko ya uwezeshaji wananchi, ambapo inadaiwa baadhi ya madiwani wakati wa kampeni za uchaguzi huzitumia kuwapa wananchi ili kuwashawishi wawachague, kisha hazirudishwi.
“Kama mwaka huo umevuna Sh. 100 Mil zitakwenda kwa vikundi 50, kila kikundi mtapata 2 Mil. ukichukua hapo kila kikundi kuna watu watano, pesa hizo wanakwenda kugawana. Mikopo kwenye mifuko hairudishwi wanajua diwani wetu katupa, ukija uchaguzi mambo yake yameyea,” amesema Mama Samia.
Mama Samia ameshauri fedha hizo zigawiwe kwa vikundi vichache vitakavyoweza kuzifanyia kazi ili zirudishwe na kutolewa kwa wengine.
“Mifuko hii ni mimi na wewe, kuwepo tena itakuja kutokana na ufanisi wa mfuko huu, ni vyema kutoa kwa vikundi vichache vinavyotambulika wakafanya kazi wakarudisha pesa ikaenda katika vikundi vingine. Kuliko kila diwani apate haijulikani zimeenda wapi,” amesema Mama Samia.
Leave a comment