Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Lugumi maji ya shingo, asalimu amri
Habari za Siasa

Lugumi maji ya shingo, asalimu amri

Said Lugumi (mwenye tai nyekundu) akitoka kwa Waziri wa Mambo ya Ndani, Kangi Lugola baada ya mazungumzo
Spread the love

MFANYABIASHARA Said Lugumi amesalimu amri kwa kukubali kukamilisha kufunga mfumo wa mashine za kielektroniki za kuchukua alama za vidole nchi nzima ndani ya miezi mine. Anaripoti Regina Kelvin…(endelea).

Lugumu ametakiwa kukamilisha mchakato huo kupitia kampuni yake ya Lugumi Enterprises.

Agizo la kukamilisha kazi hiyo limetolewa na Kangi Lugola, Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola leo tarehe 31 Julai, 2018 jijini Dar es Salaam.

Lugola amesema, baada ya kukamilisha mfumo huo Lugumi anapaswa kuukabidhi rasmi kwa Jeshi la Polisi.

“Kampuni ya Lugumi mtakumbuka moja wapo ya jambo lilimkera rais wa nchi hii. Ni kwa namna ambavyo mkataba wa mfumo wa utambuzi wa alama za vidole katika udhibiti wa uhalifu ulivyoingiwa.

“…kazi hiyo Lugumi hajaimaliza, pesa za serikali haziwezi kupotea bure. Nimemuita na amekuwa muungwana, amekuja yeye mwenyewe na nimepata fursa ya kuzungumza kwamba mfumo huu ambao umelenga kudhibiti uhalifu unakamilika,” amesema Lugolana kuongeza;

“Lugumi amekubali na ameomba tumpe miezi minne ili ahakikishe mfumo huo anaukamilisha na kuukabidhi kwa jeshi la polisi ili uweze kufanya kazi kama ilivyokusudiwa.”

Lugola kwamba, Lugumi asipokamilisha mfumo huo ndani ya miezi minne kama alivyoomba, atamfikisha kwenye mahakama ya mafisadi.

“Lakini nimemuonya kwamba kazi yangu kubwa ni kuhakikisha ile mahakama ya mafisadi ambayo imeanzishwa na Rais John Magufuli bado ina uhaba wa wateja kwa maana ya mafisadi.

“Kwa hiyo hiyo miezi minne ikikamilika na hajafanya hivyo, haraka nitahakikisha anakuwa mteja wa mahakama hiyo, hatuwezi kukubali mahakama hiyo iliyoanzishwa na rais kwa ajili ya wale wanaochezea fedha za serikali ikawa na uhaba au ikakosa wateja ilhali watu kama hawa wanazurura mitaani,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!