Friday , 2 June 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Upepo wa CCM wamtesa Lowassa
Habari za Siasa

Upepo wa CCM wamtesa Lowassa

Spread the love

EDWARD Lowassa, Wziri Mkuu Mstaafu ameonesha kuteswa na hama hama ya wapinzani kuelekea Chama Cha Mapinduzi (CCM). Anaripoti Faki Sosi…(endelea).

Lowassa ambaye ni Mjumbe Kamati Kuu ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) ameeleza kusikitishwa na kuhama kwa aliyekuwa Mbunge wa Monduli, Monduli Julias Kalanga (Chadema). Kalaga amehamia CCM usiku wa kuamkia Julai 31, 2018.

Hata hivyo Lowassa amesema, umahiri wa Chadema na moto wake kwenye Uchaguzi Mkuu ujao hauzimwi.

Lowasa kupitia taarifa yake kwa vyombo vya habari ameeleza kuwa, CCM imebadili mbinu na kuamua kurubuni wabunge na madiwani wa upinzani kutokana na ‘moto’ wa upinzani uliowashwa mwaka 2015 kwenye kampeni za uchaguzi mkuu.

“Moto ule tuliouwasha 2015 hauwezi hata mara moja kuzimwa na mbinu hizi. Wataondoka kina Kalanga wengi tu lakini kasi ya moto ule jinsi ilivyo sasa ndani ya mioyo ya Watanzania ni ya moto wa kiangazi,” amesema Lowassa na kuongeza;

“Kalanga hakuwa na sababu za msingi za kujiuzulu nafasi yake hiyo ya heshima ya kuwatumikia wananchi wa Monduli nikiwemo mimi. Uamuzi huo umetuhuzunisha na kutuumiza.

“Lakini nawaomba msife moyo hata dakika moja zaidi, kitendo hicho cha Kalanga kizidi kutupa nguvu, ari, hamasa na mori zaidi wa kuendeleza mapambano ya kuitafuta demokrasia na mabadiliko ya kweli.”

Amesema kuwa, kuhama kwenye siasa sio tukio jipya kwenye dunia hivyo sio sababu ya kurudi nyuma kwenye mapambano, “hakuna jipya katika hili, ni kawaida kwa wana siasa duniani kuhama vyama vyao na kubadilishana vijiti.”

Lowassa alihama kutoka CCM na kujiunga Chadema mwaka 2015 kisha kupewa nafasi ya kukiwakilicha chama hicho kama mgombea urais ambapo aliungwa mkono na vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA).

Vyama vinavyounda UKAWA ni pamoja na Chama cha Wananchi (CUF), Chama cha NCCR-Mageuzi, NLD na Chadema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Lusinde: CCM hatuliachii ng’o jimbo la Moshi Mjini

Spread the loveMJUMBE wa Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi (NEC), Livingston...

Habari za SiasaTangulizi

Serikali ya Mapinduzi Zanzibar: Bakharesa hajavamia shamba letu

Spread the love  IKULU Visiwani Zanzibar, imeeleza kuwa eneo la kiwanda cha...

Habari za SiasaTangulizi

Zanzibar watangaza rasmi kuwa shamba la Razaba ni mali yao

Spread the love  SERIKALI ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), imetangaza rasmi kwamba shamba...

Habari za SiasaTangulizi

Rais Mwinyi azindua Kamati ya Maridhiano Visiwani

Spread the love  RAIS wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), Dk. Hussein...

error: Content is protected !!