Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Lugola: Msitolee macho posho za polisi
Habari za Siasa

Lugola: Msitolee macho posho za polisi

Kange Lugola, Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi. Picha Ndogo IGP, Simon Sirro
Spread the love

WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola amezitaka familia za askari kutozitamani posho za chakula, badala yake watumie mishahara ya askari hao. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Lugola ametoa agizo hilo leo tarehe 14 Novemba 2018 bungeni jijini Dodoma wakati akijibu swali la Mbunge wa Kinondoni, Maulid Mtulia.

“Kweli askari wanapokwenda mafunzoni fedha zao za chakula huwafata kokote wanakokwenda, lengo la fedha kwa ajili ya lishe tunaaka jeshi lenye lishe fedha hizi lazima azitumie kama fedha za chakula.

“Natoa wito wa familia za polisi kuna wakati wanazitamani wanazikodolea macho ninaomba waziache posho hizi watumie mishahara, posho wawaachie wenyewe,” amesema Lugola.

Aidha, Lugola amesema serikali itaendelea kuhuisha posho mablimbali za askari ili ziweze kuwanufaisha.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!