Friday , 26 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Liz kukabidhiwa mikoba ya uwaziri mkuu leo
Kimataifa

Liz kukabidhiwa mikoba ya uwaziri mkuu leo

Spread the love

LIZ Truss anatarajiwa kuchukua nafasi ya Boris Johnson kama Waziri Mkuu wa Uingereza leo tarehe 6 Septemba, 2022 atakapokwenda kumuona Malkia Elizabeth huko Scotland. Anaripoti Felister Mwaipeta, TUDARCo … (endelea).

Truss mwenye umri wa miaka 47, baada ya kukabidhiwa mikoba, anatarajiwa kuteua mawaziri wa vyeo vya juu katika baraza lake la mawaziri ili kushughulikia mzozo wa kiuchumi na kuunganisha chama chake kilichogawanyika.

Truss alimshinda mpinzani wake Rishi Sunak katika upigaji kura wa wanachama wa uwongozi wa chama cha Conservative na kuahidi kupunguza kodi na kuwasaidia watu kulipa bili zao za nishati wakati Uingereza inakabiliwa na shida ya nishati inayoongezeka.

Truss alisema, “Nitachukua hatua madhubuti kutuvusha sote katika nyakati hizi ngumu ili kukuza uchumi wetu na kuibua uwezo wa Uingereza”.

Truss atamrithi Boris Johnson ambaye alilazimika kutangaza kujiuzulu mwezi Julai mwaka huu baada ya kashfa iliyoshuhudia uungwaji mkono kwa utawala wake kupungua na mawaziri kujiuzulu na kulazimika yeye kujiuzulu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

error: Content is protected !!