Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Kuelekea 2020: Ndugai aanza kumpigia chapuo Rais Magufuli
Habari za SiasaTangulizi

Kuelekea 2020: Ndugai aanza kumpigia chapuo Rais Magufuli

Rais John Magufuli (kulia) akiteta jambo na Spika wa Bunge, Job Ndugai
Spread the love

SPIKA wa Bunge, Job Ndugai, ameanza kampeni ya kumnadi Rais John Magufuli. Ameagiza kuandaliwa muswada wa Bima ya Afya kwa wote, kabla ya kufanyika uchaguzi mkuu wa mwaka 2020. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Akizungumza bungeni, Spika Ndugai alisema, “ninaeleekeza serikali, kufanya kazi usiku na mchana, ili kuandaa muswada wa Bima ya Afya kwa wote. Ninataka muswada huu, uletwe hapa bungeni na kupitishwa kabla ya mwaka 2020.” 

Spika Ndugai alitoa kauli hiyo, leo asubuhi, tarehe 4 Februari 2019, wakati wa kipindi cha maswali na majibu.

Alisema, serikali inapaswa kutoa Bima ya Afya kwa wananchi wake wote ili iwe zawadi kubwa kwa Rais Magufuli kwa wananchi wake kabla ya kufika uchaguzi mkuu ujao.

“…Wenzetu serikalini, kabla ya uchaguzi mwakani, kuwe na uwezekano wa kupatikana huduma ya afya kwa wote. Nawaomba mfanye kazi usiku na mchana kufanikisha jambo hili. Hii itakuwa zawadi kubwa kwa rais kwa wananchi wake,” ameeleza Spika Ndugai.

Aliongeza: “Tunawaomba sana jambo hili lipate msukumo wa kipekee, ili Watanzania wapate mfuko wa Bima ya Afya kwa wote.”

Kauli ya Spika Ndugai imekuja muda mfupi baada ya  Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk. Faustine Ndugulile, kuliambia Bunge kuwa “serikali iko katika mwelekeo wa kwenda kwenye mfumo wa bima moja ya afya kwa wananchi wote.”

Dk. Ndugulile amewaomba wabunge kuunga mkono muswada huo pindi utakapowasilishwa bungeni. Dk. Ndungulie alikuwa akijibu swali la msingi la mbunge wa Viti Maalum (CCM), Kiteto Koshuma.

Oktoba mwaka juzi, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano, Samia Suluhu Hassan alisema, ili kumpunguzia mzigo wa gharama za matibabu mwananchi wa kawaida, serikali imeandaa muswada wa Bima ya Afya kwa wote utakaowezesha kila mwananchi kuwa na uhakika wa matibabu.

Alitoa kauli hiyo wakati akizindua kongamano la 49 la afya jijini Dar es Salaam.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!