Wednesday , 27 September 2023
Home Kitengo Maisha Afya Wananchi watakiwa kupima afya zao mara kwa mara
Afya

Wananchi watakiwa kupima afya zao mara kwa mara

Dk. Faustin Ndungulile
Spread the love

IKIWA leo tarehe 4 Februari 2019 dunia inaadhimisha siku ya saratani, serikali imeendelea kusisitiza wananchi kupima afya zao ili kukabiliana na ugonjwa huo. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Wito huo umetolewa leo tarehe 4 Februari 2019 bungeni jijini Dodoma na Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk. Faustine Ndugulie.

Dk. Ndugulile ameeleza kuwa, watanzania wengi wenye ugonjwa wa saratani huchelewa kufika hospitali kwa ajili ya matibabu kitendo kinachopelekea kukosa tiba kwa wakati na kufariki dunia.

Amesema, takribani watu 55,000 hupata ugonjwa wa saratani kila mwaka, ambapo wanaowahi kufika hospitali kwa ajili ya vipimo na matibabu ni asimilia 25 pekee, huku asilimia 70 wakifika katika hatua za mwisho.

“ Watu 55,000 hupata saratani kwa mwaka, asilimia 25 wanawahi kufika, asilimia 70 wanafika wakiwa wamechelewa. Tunawataka Watanzania kujitokeza kwa wingi sababu kupima ni bure,” amesema Dk. Ndugulile.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

AfyaHabari Mchanganyiko

Wafanyakazi GGML wajitokeza kuchunguzwa saratani

Spread the loveWAFANYAKAZI wa Kampuni ya Geita Gold Mining Limited (GGML) leo...

AfyaHabari Mchanganyiko

GGML yatoa msaada wa vifaa tiba kuboresha afya Geita

Spread the loveKATIKA jitihada za kuendelea kuboresha sekta ya afya mkoani Geita,...

Afya

Hospitali Kanda Mtwara yaokoa mamilioni, yajipanga kuhudumia nchi jirani

Spread the love  MAMILIONI ya fedha yaliyopaswa kutumika katika kusafirisha wagonjwa kutoka...

AfyaHabari Mchanganyiko

Magonjwa yasiyoambukiza tishio, vyombo vya habari vyatakiwa kuelimisha umma

Spread the loveVYOMBO vya habari vimetakiwa kuongeza jitihada katika elimu ya kujikinga...

error: Content is protected !!