Thursday , 30 March 2023
Home Kitengo Maisha Afya Wananchi watakiwa kupima afya zao mara kwa mara
Afya

Wananchi watakiwa kupima afya zao mara kwa mara

Dk. Faustin Ndungulile
Spread the love

IKIWA leo tarehe 4 Februari 2019 dunia inaadhimisha siku ya saratani, serikali imeendelea kusisitiza wananchi kupima afya zao ili kukabiliana na ugonjwa huo. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Wito huo umetolewa leo tarehe 4 Februari 2019 bungeni jijini Dodoma na Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk. Faustine Ndugulie.

Dk. Ndugulile ameeleza kuwa, watanzania wengi wenye ugonjwa wa saratani huchelewa kufika hospitali kwa ajili ya matibabu kitendo kinachopelekea kukosa tiba kwa wakati na kufariki dunia.

Amesema, takribani watu 55,000 hupata ugonjwa wa saratani kila mwaka, ambapo wanaowahi kufika hospitali kwa ajili ya vipimo na matibabu ni asimilia 25 pekee, huku asilimia 70 wakifika katika hatua za mwisho.

“ Watu 55,000 hupata saratani kwa mwaka, asilimia 25 wanawahi kufika, asilimia 70 wanafika wakiwa wamechelewa. Tunawataka Watanzania kujitokeza kwa wingi sababu kupima ni bure,” amesema Dk. Ndugulile.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

AfyaHabari

Ugonjwa wa ajabu ulioua watano Bukoka ni Marburg

Spread the loveWAZIRI wa Afya, Ummy Mwalimu amesema ugonjwa wa ajabu uliosababisha...

AfyaHabariHabari

Ugonjwa wa ajabu wadaiwa kuua watano Kagera, Serikali yatoa tahadhari

Spread the loveJUMLA ya watu watano wanaidaiwa kufariki dunia  katika vijiji vya...

Afya

LHRC yapinga kufutwa Toto Afya: Ni ukiukaji wa sheria za watoto

Spread the love  KITUO cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) kimekosoa...

Afya

Manesi 7 mbaroni tuhuma za kuwauzia dawa wagonjwa usiku wa manane

Spread the love  JUMLA ya wauguzi/manesi saba wa Hospitali ya Manispaa ya...

error: Content is protected !!